Muharram (kwa Kiarabu: محرم ) ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiislamu.
Ni kati ya miezi minne mitakatifu ya mwaka.
Jina la mwezi limetokana na neno "haram" yaani "mwiko" au "kukatazwa" kwa maana ya kwamba vita haitakiwi mwezi huo.
Siku ya kwanza ya Muharram ni Mwaka Mpya wa Kiislamu.
Sikukuu ya Ashura iko tarehe 10 Muharram. Hasa Waislamu Washia hukumbuka kifo cha Hussein ibn Ali (mjukuu wa Mtume Muhammad anayeheshimiwa kama Imamu wa Washia) kwenye mapigano ya Kerbela.
Kwa jumla Washia wanaangalia Muharram kama mwezi wa huzuni na katika mazingira yenye Washia wengi kuna mikutano mingi ya kidini ambako historia ya Ashura na kifo cha Hussein inakumbukwa kuanzia siku ya kwanza hadi ya kumi ambayo ni Ashura.
Kati ya Wasunni siku ya Ashura inatazamwa kama siku ya saumu hasa..
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Muharram, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.