Maneno saba katika Ukristo ni yale ambayo Yesu aliyatamka akiwa msalabani na yamerekodiwa katika Injili nne.
Kati yake, matatu yanapatikana katika Injili ya Luka tu, mawili katika Injili ya Yohane tu. Lingine linapatikana katika Injili ya Mathayo na Injili ya Marko vilevile. Lingine tena limerekodiwa na Yohane lakini Mathayo na Marko wamelidokeza.
Katika Mathayo na Marko, Yesu Kristo anamlilia Mungu. Katika Luka, yeye anawasamehe wauaji wake, anamfariki mhalifu aliyetubu, na kumkabidhi Baba roho yake. Katika Yohane, Yesu anasema na mama yake na mwanafunzi mpendwa, anatokeza kiu yake, na kutangaza utimilifu wa kazi na maisha yake yote kadiri ya mpango wa Mungu.
Maneno ya buriani ya mtu yeyote yanatiwa maanani sana. Yanaweza kusaidia kuelewa nini ilikuwa muhimu kwake. Ilikuwa hivyo hasa kwa Yesu aliyeweza kusema machache tu kutokana na hali yake.
Tangu karne ya 16 maneno hayo yametumika sana katika mahubiri ya madhehebu mbalimbali siku ya Ijumaa kuu, na vitabu vingi vimetungwa kuyafafanua.
Watunzi mbalimbali waliyatia katika muziki.
Mpangilio wa kawaida ni huu:
Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Maneno saba kama historia yake au athari wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Maneno saba, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.