Wema Abraham Sepetu (alizaliwa 28 Septemba 1988) ni mwanamitindo, mjasiriamali na mwigizaji kutoka nchini Tanzania.
Aliwahi kuwa Miss Tanzania kwa mwaka wa 2006. Aliiwakilisha Tanzania katika Miss Dunia 2006, ambayo ilifanyika nchini Poland. Baadaye alikua mwigizaji nchini Tanzania.
Wema ni mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne wa mwanadiplomasia Abraham Sepetu. Alianza elimu ya msingi na hadi sekondari amesomea katika shule moja tu iitwayo "Academic International" iliyopo maeneo ya Mikocheni, jijini Dar es Salaam. Pamoja na yote hayo, binti huyu amelelewa na kuishi kama mtu wa Magharibi. Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Ubunifu wa Teknolojia cha Limkokwing nchini Malaysia kusoma kozi ya biashara za kimataifa ambayo alisoma kwa mwaka mmoja, kisha akakatisha masomo ili kuendelea na uigizaji.
Kipaji zaidi cha Wema kiligundulika katika sanaa ya filamu, ambapo alifanikiwa kucheza vema kabisa katika filamu A Point of No Return akishirikiana na mchezaji filamu maarufu wa Kitanzania Steven Kanumba.
Wema alivishwa pete ya uchumba na msanii maarufu wa Bongo Flava Diamond Platnumz, lakini kwa sasa wameshaachana.
Pia Wema amekuwa akijulikana kwa kuwa na sauti ndogondogo.
Baada ya kushinda taji la Miss Tanzania mnamo 2006, Wema alisafiri kwenda Warsaw, Poland kushindana katika kinyanganyiro cha Miss World 2006, hata hivyo hakufanikiwa kuingia katika kumi na saba bora.
Mnamo mwaka 2013 alizindua kampuni yake kwa jina la Endless Fame Production. Shirika hilo linahusika na utengenezaji wa sinema na Usimamizi wa wasanii, wameweza kusimamia baddhi ya wanamuziki wa Kitanzania kama vile Mirror na Ally Luna. Shirika hilo limetengeneza sinema kama vile Supestar, Unexpected, Day After Death, Family, and Heaven Sent.
Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wema Sepetu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Wema Sepetu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.