Antioko IV wa Syria alijiita Epifane (kwa Kigiriki Ἀντίοχος Ἐπιφανής) akitaka kujitambulisha kama tokeo la mungu mmojawapo.
Lakini watu walimuita Epimane, yaani kichaa, kutokana na madai yake yasiyo na kiasi.
Aliishi miaka 215 KK – 164 KK akitawala dola la Waseleuki kuanzia mwaka 175 KK hadi kifo chake.
Juhudi zake za kueneza ustaarabu wa Ugiriki wa kale kati ya Wayahudi zilishindwa na Wamakabayo waliopigania uhuru wa dini kama inavyosimuliwa katika kitabu cha kwanza cha Wamakabayo na kitabu cha pili cha Wamakabayo (ambavyo ni kati ya Deuterokanoni).
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Antioko Epifane, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.