Jenasi 5:
Komba | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Komba magharibi (Galago senegalensis) | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
|
Komba ni wanyama wadogo wa familia Galagidae. Wamo miongoni mwa wanyama wa asili wa jamaa ya binadamu. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara.
Hukiakia usiku na hulala mchana katika matundu ya miti. Kwa ajili hiyo wana macho makubwa ili kuona vizuri kwenye giza. Hata masikio yao ni makubwa ili kusikia mawindo yao na hata maadui wao. Mkia mrefu wao huzuia wasiyumbe wakitembea juu ya matawi. Wanaweza kuruka sana, hadi mita 2 kwa wima. Wana makucha kama yale ya watu, isipokuwa lile la kidole cha pili cha miguu ambao ni mrefu wenye ncha kali na hutumika kwa kusafisha manyoya. Hula wadudu, wanyama wadogo, matunda na sandarusi.
Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wiki: WikiProject Mammals/Article templates/doc.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Komba, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.