Kalenda Ya Ethiopia

Kalenda ya Ethiopia (kwa Kiamhari: የኢትዮጵያ ዘመን አቆጣጠር ye'Ityoṗṗya zemen aḳoṭaṭer) ni kalenda rasmi nchini Ethiopia na pia kalenda inayotumiwa na Wakristo walio wengi nchini Eritrea.

Asili yake ni kalenda ya Wakopti kwa sababu Kanisa la Ethiopia kwa karne nyingi lilikuwa kama tawi la kanisa la Kikopti la Misri.

Miezi 13 na miaka mirefu

Kalenda huwa na mwaka wa miezi 13; miezi kamili 12 ya siku 30 na mwezi wa 13 mfupi wa siku 5 yaani jumla siku 365. Kila mwaka wa 4 ni mwaka mrefu ambako mwezi wa 13 huwa na siku 6 yaani siku 366 kwa jumla. Chanzo cha mwaka kinalingana na 11 Septemba ya kalenda ya Gregori (kalenda ya kimataifa), isipokuwa baada ya mwaka mrefu kinalingana na 12 Septemba na tofauti inasawazishwa katika mwaka mrefu wa kalenda ya Gregori.

Tofauti na kalenda ya Gregori utaratibu wa mwaka mrefu kila mwaka wa nne unaendelea bila kituo.

Hesabu ya miaka

Hesabu ya miaka ni tofauti na mwaka wa Gregori kiasi cha miaka 7-8. Sababu yake ni ykwamba kalenda hii, sawa na ya Wakopti, hufuata makadirio ya mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu ambayo ni tofauti kidogo na hesabu ya magharibi inayomfuata Dionysius Exiguus. Kati ya Januari hadi 10/11 Septemba tofauti ni miaka 8, kwa miezi inayobaki tofauti ni miaka 7. Kwa hiyo mwaka 2007 ya kalenda ya kimataifa ililingana na mwaka 2000 wa Ethiopia.

Miezi

Ge'ez, Kiamhari na Kitigrinya Kikopti Chanzo cha mwaka
katika kalenda ya Gregori
Chanzo cha mwaka
baada ya mwaka mrefu
Mäskäräm (መስከረም) Tut 11 Septemba 12 Septemba
Ṭəqəmt(i) (ጥቅምት) Babah 11 Oktoba 12 Oktoba
Ḫədar (ኅዳር) Hatur 10 Novemba 11 Novemba
Taḫśaś ( ታኅሣሥ) Kiyahk 10 Desemba 11 Desemba
Ṭərr(i) (ጥር) Tubah 9 Januari 10 Januari
Yäkatit (Tn. Läkatit) (የካቲት) Amshir 8 Februari 9 Februari
Mägabit (መጋቢት) Baramhat 10 Machi 10 Machi
Miyazya (ሚያዝያ) Baramundah 9 Aprili 9 Aprili
Gənbot (ግንቦት) Bashans 9 Mei 9 Mei
Säne (ሰኔ) Ba'unah 8 Juni 8 Juni
Ḥamle (ሐምሌ) Abib 8 Julai 8 Julai
Nähase (ነሐሴ) Misra 7 Agosti 7 Agosti
Ṗagʷəmen/Ṗagumen (ጳጐሜን/ጳጉሜን) Nasi 6 Septemba 6 Septemba

Marejeo

  • "The Ethiopian Calendar", Appendix IV, C.F. Beckingham and G.W.B. Huntingford, The Prester John of the Indies (Cambridge: Hakluyt Society, 1961).
  • Ginzel, Friedrich Karl, "Handbuch der matematischen und technischen Chronologie", Leipzig, 3 vol., 1906-1914

Viungo vya Nje

Kalenda Ya Ethiopia  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kalenda ya Ethiopia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

Kalenda Ya Ethiopia Miezi 13 na miaka mirefuKalenda Ya Ethiopia Hesabu ya miakaKalenda Ya Ethiopia MieziKalenda Ya Ethiopia MarejeoKalenda Ya Ethiopia Viungo vya NjeKalenda Ya EthiopiaAsiliEritreaEthiopiaKalendaKanisa la KikoptiKanisa la Kiorthodoksi la EthiopiaKarneKiamhariMisriWakristo

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

MwanaumeLughaUhuru wa TanganyikaSerikaliUsafi wa mazingiraUkristo nchini TanzaniaSimba (kundinyota)Kinembe (anatomia)Mkoa wa RukwaIniJakaya KikweteMvuaBiasharaMohamed HusseinSarangaVita Kuu ya Kwanza ya DuniaKaswendeTetemeko la ardhiWilaya ya KinondoniTarbiaNgono zembeSakramentiMofolojiaMkoa wa DodomaMJTulia AcksonMnyamaMohammed Gulam DewjiWilaya ya IlalaMadhara ya kuvuta sigaraNangaVielezi vya namnaTabianchi ya TanzaniaStafeliMkoa wa ArushaKiimboMalariaKito (madini)LenziVita ya uhuru wa MarekaniHistoria ya uandishi wa QuraniP. FunkMagonjwa ya kukuSaida KaroliNomino za pekeeFani (fasihi)24 ApriliLigi Kuu Tanzania BaraLugha ya maandishiNenoShinikizo la juu la damuMaumivu ya kiunoRisalaTafsidaMkataba wa Helgoland-ZanzibarSemiMajira ya baridiBendera ya TanzaniaMfumo wa JuaMuungano wa Madola ya AfrikaSoko la watumwaAfrika Mashariki 1800-1845MandhariUbongoAina za ufahamuPopoJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaUenezi wa KiswahiliNimoniaMauaji ya kimbari ya RwandaVita vya KageraOrodha ya Marais wa Zanzibar🡆 More