Mwaka mpya ni siku ya kwanza ya mwaka na mara nyingi ni sherehe na nafasi ya watu kutakiana heri na baraka za mwaka mpya.
Kalenda ya Gregori | 2024 MMXXIV |
Kalenda ya Kiyahudi | 5784 – 5785 |
Ab urbe condita (Roma ya Kale) | 2777 |
Kalenda ya Ethiopia | 2016 – 2017 |
Kalenda ya Kiarmenia | 1473 ԹՎ ՌՆՀԳ |
Kalenda ya Kiislamu | 1446 – 1447 |
Kalenda ya Kiajemi | 1402 – 1403 |
Kalenda za Kihindu | |
- Vikram Samvat | 2079 – 2080 |
- Shaka Samvat | 1946 – 1947 |
- Kali Yuga | 5125 – 5126 |
Kalenda ya Kichina | 4720 – 4721 癸卯 – 甲辰 |
Katika tamaduni mbalimbali nafasi hii ni sikukuu moja au zaidi pasipo na kazi za kawaida.
Tarehe ya mwaka mpya inategemea kalenda yake. Kuna kalenda tofautitofauti zinazotumiwa dunani na kila moja ina mwaka wake wa pekee pamoja na siku tofauti ya kuanza, mfano kalenda yya kiraia, kalenda ya Kiislamu, mwaka wa Kanisa.
Kalenda inayotumiwa zaidi kimataifa ni Kalenda ya Gregori na hapa mwaka mpya ni 1 Januari.
Uajemi, Afghanistan, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Tajikistan, Azerbaijan, Turkmenistan na Kashmir husheherekea mwaka mpya kufuatana na kalenda ya Kiajemi kwenye sikukuu ya Nouruz ambayo ni sawa na sikusare ya machipuo inayotokea kati ya tarehe 20 - 21 Machi kwenye kalenda ya Gregori lakini kwao mwezi na mwaka mpya unaanza
Wachina na Wavietnam husheherekea mwaka mpya wakati wa mwezi mwandamo wa pili baada ya solistasi ya Desemba na tarehe hii inatokea kati ya 21 Januari na 21 Februari.
Nchi ya Israeli na Wayahudi husheherekea mwaka mpya kufuatana na Kalenda ya Kiyahudi kwa jina la Rosh Hashana ambayo ni siku inayotokea kati ya Septemba na nusu ya kwanza ya Oktoba.
Waislamu na nchi ya Saudia huwa na mwaka mpya kufuatana na kalenda ya Kiislamu. Kalenda hii inafuata Mwezi si Jua na kwa hiyo sikuu zake huzunguka katika mwaka wa jua. Hakuna desturi ya kusheherekea mwaka mpya wa Kiislamu.
Sikukuu ya Diwali inasheherekewa na jumuiya kadhaa za Wahindu pia kama mwaka mpya.
Nje ya mahesabu haya kuna kalenda nyingine zisizoanzisha mwaka kwa sherehe. Mifano ni:
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mwaka mpya kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mwaka mpya, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.