Waadventisti ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali yanayosisitiza ujio wa pili wa Yesu yakisema uko jirani kutokea.
Ingawa sisitizo hilo lilijitokeza mara kadhaa katika historia ya Kanisa, lilipata nguvu mpya huko Marekani katika karne ya 19.
William Miller ndiye anayetajwa kama mwanzilishi wa tapo hilo kwa kufanya watu kati ya 50,000 na 100,000 kutarajia ujio huo utatokea tarehe 22 Oktoba 1844.
Baada ya siku hiyo kupita kama kawaida, wengi waliachana na utabiri huo, wengine walianzisha makundi mbalimbali. Miller hakujiunga na lolote, bali alihimiza umoja hadi kifo chake (1849).
Kati yake, lililoenea zaidi ni lile la Waadventista Wasabato (mwanzo rasmi mwaka 1863) ambalo kwa sasa lina waumini zaidi ya 17 milioni duniani kote.
Mashahidi wa Yehova pia wana asili katika tapo hilo.
Jaribio la kutabiri tarehe ya ujio wa pili kwa kupiga hesabu kutokana na Biblia lilitokea tena na tena hadi karne ya 21 bila mafanikio.
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Waadventisti kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Waadventisti, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.