Trigonometria

Trigonometria (kutoka Kigiriki trigonon = pembetatu na metron = kipimo, upimaji) ni sehemu ya jiometria, hivyo ni tawi la hisabati.

Inatazama habari za pembetatu na uhusiano kati ya pande na pembe. Uhusiano kati ya urefu wa pande na ukubwa wa pembe hufuata kanuni fulani na kwa kujua kanuni hizo inawezekana kukadiria umbali wa kitu au ukubwa la eneo kwa kujua habari chache tu.

Elimu hiyo ilitokea wakati wa utamaduni wa Ugiriki ya Kale wakati wataalamu walifanya utafiti wa nyota na kukadiria umbali wa nyota na dunia. Walitambua kanuni za trigonometria kwa mfano wa pembetatu mraba. Ilhali kila pembetatu inaweza kugawiwa kwa pembetatu mraba mbili, elimu hiyo inatosha kujibu maswali mengi.

Kwa kawaida trigonometria inatazama maumbo bapa lakini kuna pia trigonometria ya tufe, yaani kuangalia pembetatu zilizopo usoni wa tufe au mpira.

Misingi

Trigonometria 
Pembetatu na pande / pembe zake katika trigonometria.

Trigonometria inafuata hasa kanuni za pembetatu mraba, yaani pembetatu ambako pembe moja ina nyuzi 90°.

Jumla ya pembe 3 za pembetatu daima ni nyuzi 180°. Kwa hiyo kama pembe moja ni pembemraba (=90°) zile mbili nyingine ni pembe kali ambazo kwa jumla zina pia nyuzi 90 maana ni vikamilisho pembemraba.

Kwa hiyo kama pembe moja ya pembetatu ina nyuzi 90° na moja nyingine kati ya pembe tatu inajulikana basi hata ukubwa wa pembe ya tatu si siri tena.

Mara viwango vya pembe vinapojulikana tunaweza pia kujua uhusiano wa urefu baina ya pande. Kwa hiyo kama urefu wa upande mmoja unajulikana inawezekana kutaja urefu wa pande nyingine pia.

Majina yafuatayo hutumiwa katika trigonometria kwenye pembetatu mraba:

  • Pembetatu mraba huwa na pande a, b, c. Kona zaitwa A, B, C. Pembe ni α, β, γ ambayo hutajwa kwa herufi za Kigiriki alfa, beta na gamma. Katika mfano huu γ ni pembemraba.
  • Hipotenusi (ing. hypotenuse) ni upande kinyume cha pembemraba, hii ni pia upande mrefu. Katika mfano kwenye picha ni upande c.
  • Majina ya pande nyingine yanategemea pembe husika. Katika mfano wa picha pembe husika imeteuliwa kuwa α kwa hiyo "mkabala wa alfa" (ing. opposite) ni upande kinyume cha α. "Tangamani ya alfa" (ing. adjacent) ni upande unaoanza kwenye kona A ya α lakini si hipotenusi. Vivyo hivyo mkabala wa β ni upande "b" na tangamani ya β ni upande "a".

Fomula husisho za trigonometria

Kuna fomula husisho (ing. functions) tatu kwa pembetatu mraba katika trigonometria. Pamoja na husisho kinyume (ing. "reciprocals") kuna sita kwa jumla.

Sini (ing. sine, sinus, kifupi sin) - Sini ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Kosini (ing. cosine, cosinus, kifupi cos) - Kosine ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Tanjenti (ing. tangent, kifupi tan) - Tanjenti ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Husisho kinyume za husisho hizi ni:

Kosekanti (ing. cosecant, kifupi csc) - Kosekanti ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Sekanti (ing. secant, kifupi sec) - Sekanti ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Kotangenti (ing. cotangent, kifupi cot) - Kotangenti ya pembe ni sawa na Trigonometria 

Marejeo

Viungo vya nje

Trigonometria  Makala hii kuhusu mambo ya hisabati bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Trigonometria kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

Trigonometria MisingiTrigonometria Fomula husisho za trigonometriaTrigonometria MarejeoTrigonometria Viungo vya njeTrigonometriaHisabatiJiometriaKigirikiTawi

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Bikira MariaUti wa mgongoWairaqwKishazi tegemeziMuundo wa inshaNdotoMorokoTaswira katika fasihiAlomofuArusha (mji)Uvimbe wa koromeo usababishwao na streptokokiSemantikiMmeaJiniMahariMkoa wa GeitaUturukiOrodha ya makabila ya TanzaniaHistoria ya KiswahiliP. FunkKukiKuzimuMagonjwa ya machoTido MhandoAfrika ya Mashariki ya KijerumaniUtataHektariAthari za muda mrefu za pombeWilaya ya BuchosaMkoa wa RuvumaOrodha ya mapapaKiunzi cha mifupaMhandisiQR codeNafsiTambikoMavaziAbrahamuIraqTanganyika (ziwa)KakakuonaMarekaniMkoa wa ManyaraOrodha ya Waandishi wa TanzaniaAllahMkoa wa MbeyaTetekuwangaBeno KakolanyaKamusi Hai ya Kiswahili MtandaoniKiimboChuiSalama JabirHistoria ya UislamuNyokaVolkenoWaheheUshairiMkoa wa GifuMkondo wa umemeIsimuMafumbo (semi)Mmeng'enyoIVivumishi ya kuulizaKaswendeKata za Mkoa wa Dar es SalaamMizimuUkomaVita Kuu ya Pili ya DuniaWangoniBaraza la mawaziri TanzaniaSamliIbadaHali maadaNenoZiwa ViktoriaMrisho Mpoto🡆 More