Saksonia-Anhalt (Kijerumani: Sachsen-Anhalt) ni moja ya majimbo 16 ya kujitawala ya Ujerumani lenye wakazi milioni 2,3 kwenye eneo la 20 446 km².
Mji mkuu ni Magdeburg. Waziri mkuu ni Reiner Haseloff (CDU).
Saksonia-Anhalt imepakana na majimbo ya Ujerumani ya Mecklenburg-Pomerini, Brandenburg, Saksonia, Thuringia, Hesse na Saksonia ya chini.
Miji mikubwa ni pamoja na Magdeburg, Halle (Saale) na Dessau.
Elbe na Saale ni mito muhimu zaidi.
Kaskazini ya jimbo ni nchi tambarare; katikati kuna maeneo ya rutba kubwa katika mazingira ya Magdeburg. Kusini ni eneo la vilimavilima vinavyopanda juu hadi milima ya Harz.
Jimbo la Saksonia Anhalt lilianzishwa mwaka 1945 kwa kuunganisha maeneo mawili: Mkoa wa Saksonia (Sachsen) wa Prussia na jimbo la Anhalt. 1949 likawa sehemu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani (Ujerumani ya Mashariki). Kutokana na harakati ya kubadilisha utawala katika Ujerumai ya Mashariki jimbo liligawiwa kuwa mikoa 2 ya Halle und Magdeburg na jimbo lilifutwa.
Wakati wa maungano ya Ujerumani mikoa ya awali ilibatilishwa na jimbo la Sachsen-Anhalt liliundwa tena mwaka 1990.
Makala hii kuhusu maeneo ya Ujerumani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Saksonia-Anhalt kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Baden-Württemberg • Bavaria (Bayern) • Berlin • Brandenburg • Bremen • Hamburg • Hesse (Hessen) • Mecklenburg-Pomerini Magharibi (Mecklenburg-Vorpommern) • Saksonia Chini (Niedersachsen) • Rhine Kaskazini-Westfalia (Nordrhein-Westfalen) • Rhine-Palatino (Rheinland-Pfalz) • Saar (Saarland) • Saksonia (Sachsen) • Saksonia-Anhalt (Sachsen-Anhalt) • Schleswig-Holstein • Thuringia (Thüringen) |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Saksonia-Anhalt, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.