Ngano nyekundu (lat.
Ngano nyekundu (Secale cereale) | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Ngano nyekundu | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
|
Mbegu au punje za ngano nyekundu ni nafaka ambayo ni chakula muhimu katika sehemu za dunia hasa kwenye kanda zisizo na joto au baridi kali. Ni mmea ulio karibu na ngano.
Matumizi yake ni kwa ajili ya unga, mkate, bia, aina za wiski na pombe mbalimbali halafu lishe ya wanyama.
Ngano nyekundu hustawi kwenye ardhi ya mchanga ambako ngano haiendelei vizuri inavumilia pia tofauti kubwa zaidi za mvua na ukame kuliko ngano.
Nchi walima wakuu wa ngano nyekundu — 2005 (millioni t³) | |
---|---|
Urusi | 3.6 |
Poland | 3.4 |
Ujerumani | 2.8 |
Belarusi | 1.2 |
Ukraine | 1.1 |
China | 0.6 |
Kanada | 0.4 |
Uturuki | 0.3 |
Marekani | 0.2 |
Austria | 0.2 |
Dunia | 13.3 |
Habari za FAO |
Ngano nyekundu hulimwa hasa katika nchi za Ulaya ya Mashariki, ya kati na kaskazini kama vile Ujerumani, Poland, Ukraine, Belarusi, Lithuania, Latvia hadi Urusi. Hulimwa pia katika Amerika ya Kaskazini (Kanada na Marekani), katika Amerika Kusini (Argentina), Uturuki, Kazakhstan na China ya kaskazini.
Katika Afrika imelimwa kidogo kwenye nyanda za juu za Tanzania pia Kenya.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ngano nyekundu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.