Mtaalamu wa anga ni mtaalamu wa masuala ya elimuanga (kwa Kiingereza: astronomy) au elimu ya anga-nje na violwa vya angani kama nyota, sayari, nyotamkia, na galaksi.
Kihistoria watu hao walitumia muda mwingi kuangalia nyota za anga kwa msaada wa vyombo kama darubini. Leo hii wataalamu wa anga hutumia hasa kompyuta na data kutokana na vipimo vya paoneaanga, vyombo vya anga-nje na darubini za angani.
Wataalamu wa anga wamesoma elimuanga ambayo ni tawi la pekee la sayansi, mara nyingi pamoja na kusoma matawi mengine ya sayansi kama fizikia, kemia, biolojia na kadhalika.
Wasichanganywe na majusi ambao husomea unajimu (kwa Kiingereza: astrology) na kutoa utabiri kuhusu maisha na tabia za watu kwa kuwa huo si tawi la sayansi yoyote, ingawa unadai kutegemea uchunguzi wa nyota n.k.
Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mtaalamu wa anga kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mtaalamu wa anga, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.