Misuli ni sehemu ya mwili wa wanyama na binadamu inayowezesha mwendo wa viungo vyake.
misuli inaundwa na tishu ya pekee yenye uwezo wa kujinywea na kulegea. Wakati wa kujinywea huwa mifupi zaidi. Kwa njia hii misuli inayounganishwa na mifupa ya mkono au mguu huleta mwendo wa viungo hivi.
Misuli hutofautishwa kwa namna mbalimbali:
Mara nyingi hutofautishwa namna tatu za misuli:
Misuli ya kiunzi na moyo huitwa pia "misuli milia" kutokana na milia inayoonekana usoni mwao. Milia hii inatokana na muundo wa misuli hii inayofanywa na vinyuzi virefu vya rangi mbili vinavyopangwa taratibu katika misuli na kuonyesha milia meupe na mekundu kwa kubadilishana. Vinyuzi vyekundu ni protini za kiaktini na vinyuzi vyeupe ni protini kimiosi.
Misuli inaundwa na seli za pekee zenye uwezo wa unyweo. inatekeleza unyweo baada ya kupokea kiamshi kupitia neva. Kiamshi ni mshtuko wa umeme unaopitishwa kutoka seli kwenda seli nyingine. Seli za misuli huwa na protini za kiaktini na kimiosini.
Wakati misuli inapokea kiamshi kutoka neva nafasi katika utando wake inapitisha kalsi na kalsi inasababisha aina mbili za protini kuingiliana hivyo kufupisha urefu wa misuli.
Makala hii kuhusu mambo ya anatomia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Musuli kama matumizi yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Musuli, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.