Dennis Coles (amezaliwa tar.
9 Mei 1970) ni msanii wa muziki wa hip hop kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Ghostface Killah. Huyu ni mmoja kati ya wanaounda kundi zima la Wu-Tang Clan. Baada ya kundi kuambulia mafanikio yake makubwa kwa kutoa albamu yao ya kwanza iliyokwenda kwa jina la Enter the Wu-Tang (36 Chambers) , huyu bwana naye akaamua kujiendeleza mwenyewe akiwa kama msanii wa kujitegemea na kuweza kupata mafanikio kibao. Ghostface Killah akatoa albamu yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina la Ironman, ambayo ilipokewa vyema sana na watathmini wa masuala ya muziki. Akaendeleza kazi yake, na kutengeneza albamu zake zilizojishindia tuzo kemekem. Albamu hizo ni pamoja na Supreme Clientele, Fishscale, na The Big Doe Rehab.
Ghostface Killah | |
---|---|
| |
Maelezo ya awali | |
Jina la kuzaliwa | Dennis Coles |
Pia anajulikana kama | Tony Starks, Ironman, General Tony Starks, Pretty Toney, The Wallabee Kingpin, GFK, Ghost Deini, Starky Love, P Tone, Sun God, Wally Champ |
Amezaliwa | 9 Mei 1970 |
Asili yake | Staten Island, New York, Marekani |
Aina ya muziki | Hip hop |
Miaka ya kazi | 1991–mpaka sasa |
Studio | Razor Sharp, Epic, Starks Enterprises, Def Jam |
Ame/Wameshirikiana na | Wu-Tang Clan, Theodore Unit, MF DOOM, Rakim, Adult Swim |
Tovuti | Ghostface's official site |
Ghostface Killah ni maarufu mno kwa staili yake ya sauti kubwa, kuchana kwa haraka-haraka, na staili yake ya kuimba kama hataki huku akiwa anatia mbwembwe za maneno ya kitaa-kistori fulani ya kujitambua.
Ghostface Killah amezaliwa na kukulia mjini Stapleton kwenye nyumba za miradi huko New York. Kwenye wimbo wake wa kujielezea mwenyewe wa "All That I Got Is You", Ghost anaelezea maisha yake ya utoto. Ana rap akielezea jinsi alivyokua kwenye mjengo wa vyumba vitatu vya kulalia bila baba yake, ambaye alimwacha tangu akiwa na umri wa miaka sita.
Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Marekani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ghostface Killah kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ghostface Killah, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.