Edmond Halley (8 Novemba 1656 - 14 Januari 1742) alikuwa mwanaastronomia kutoka nchini Uingereza.
Alikuwa pia mtaalamu wa hisabati, wa metorolojia na wa fizikia. Halley anajulikana zaidi kwa kukadiria obiti ya nyotamkia iliyopata jina lake, yaani Nyotamkia ya Halley .
Halley alizaliwa katika kaunti ya Middlesex, Uingereza. Babake Edmond Halley alikuwa fundi wa sabuni mjini London na tajiri. Aliposoma shuleni kijana Halley alivutwa sana na hisabati. Alisoma shule ya St Paul's alipoanza kujifunza astronomia. 1673 aliingia Queen's College mjini Oxford. Wakati bado alikuwa mwanafunzi, Halley alitunga makala kuhusu Mfumo wa Jua na madoa ya Jua.
Pale Oxford Halley alifahamiana na mwanaastronomia mashuhuri John Flamsteed aliyekuwa akikusanya habari za nyota zote zilizoweza kutazamiwa kwenye angakaskazi na kuandaa orodha ya namba za Flamsteed. Halley alijitolea kufanya kazi ileile kwa ajili ya angakusi.
Mnamo mwaka 1676, alipokuwa na umri wa miaka 20, aliondoka katika Oxford akasafiri kwenda kisiwa cha St Helena katika Atlantiki ya kusini akaanzisha paoneaanga na kuchunguza nyota akaweza kuorodhesha nyota 341 za angakusi. Mafanikio haya yalimpatia shahada ya uzamili (MA).
Kwenye Septemba 1682 alitazama nyota yenye mendo kwenye aliyotambua kuwa ni nyotamkia ailiyowahi kutazamiwa. Alitabiri kurudi kwake mnamo mwaka 1758. Halley mwenyewe aliaga dunia kabla ya marudio lakini wataalamu wa wakati walikumbuka utabiri wake n hivyo nyotamkia hii iliyoendelea kurudi ilipata jina lake.
Mnamo 1686, Halley alichapisha sehemu ya pili ya matokeo kutoka kwa msafara wake wa St. Helena . Hii ilikuwa makala kuhusu upepo na monsuni. Hapa alitambua ni joto la Jua linalosababisha miendo katika angahewa. Aliatambua uhusiano baina kanieneo angahewa jinsi inavyopinwa kwa barometa na kimo juu ya usawa wa bahari . Halley pia alimshawishi Sir Isaac Newton kuchapisha kitabu kuhusu uvumbuzi wake wa graviti .
Mnamo 1691 Halley alitafuta nafasi ya Profesa wa astronomia katika Chuo Kikuu cha Oxford . Kwa vile alikuwa anajulikana kama mkanaji Mungu, alipingwa na Askofu Mkuu wa Canterbury, John Tillotson halafu hakuchaguiwa.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Edmond Halley, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.