Nguchiro

Jenasi 13:

Nguchiro
Nguchiro mwembamba (Galerella sanguinea)
Nguchiro mwembamba (Galerella sanguinea)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Carnivora (Wanyama mbua)
Nusuoda: Feliformia (Wanyama kama paka)
Familia: Herpestidae (Wanyama walio na mnasaba na Nguchiro)
Bonaparte, 1845
Ngazi za chini

Usambazaji wa nguchiro (kuna spishi zaidi ambapo rangi ni nzito zaidi)
Usambazaji wa nguchiro (kuna spishi zaidi ambapo rangi ni nzito zaidi)

Nguchiro (Kiing. mongoose) ni wanyama wadogo kiasi wa familia Herpestidae. Kuna spishi nne huko Madagaska ziitwazo nguchiro pia (nguchiro-bukini) na ambazo ziliainishwa katika Herpestidae, lakini malinganisho ya ADN yameonyesha kwamba spishi hizi zina mnasaba zaidi na spishi za Eupleridae. Sasa zimepewa nusufamilia yao binafsi Galidiinae. Nguchiro wa kweli wanatokea Afrika, Asia na Ulaya ya kusini. Wamewasilishwa katika visiwa kadhaa vya Karibi na Hawaii ambapo wamekuwa usumbufu.

Wanyama hawa ni warefu na wembamba na wana mkia mrefu wenye manyoya mengi. Wanafanana na chororo lakini wako wakubwa zaidi. Rangi yao ni hudhurungi, kahawia, kijivu au nyeusi. Wao ni wanyama mbua na hula wadudu, kaa, nyungunyungu, mijusi, nyoka, ndege na wagugunaji, na mara nyingi mayai na mizoga pia. Nguchiro hujulikana kwa uwezo wao wa kuua nyoka na kukinga sumu yao. Huishi peke yao au kwa makundi (k.m. nguchiro miraba na nguchiro-jangwa) na hukiakia mchana lakini pengine usiku pia.

Spishi za Afrika

Spishi za mabara mengine

Picha

Soma pia

Nguchiro 
WikiMedia Commons
Wiki Commons ina media kuhusu:
  • Rasa, Anne (1986). Mongoose Watch: A Family Observed. Garden City, NY: Anchor Press/Doubleday & Co. 
  • Hinton, H. E. & Dunn, A. M. S. (1967). Mongooses: Their Natural History and Behaviour. Berkeley: University of California Press. 

Tags:

Nguchiro Spishi za AfrikaNguchiro Spishi za mabara mengineNguchiro PichaNguchiro Soma piaNguchiro

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

BaruaWapareNyanda za Juu za Kusini TanzaniaUhifadhi wa fasihi simuliziTabiaBikiraMaliNyanya chunguMivighaMapambano kati ya Israeli na PalestinaIstilahiSintaksiec4tgMkoa wa SongweReal MadridLuhaga Joelson MpinaNjia ya MachoziJiniTafsidaMikoa ya TanzaniaHistoria ya ZanzibarJumuiya ya MadolaUhalifu wa kimtandaoAfrika KusiniKichochoHoma ya manjanoSaidi Salim BakhresaOrodha ya viwanja vya michezo TanzaniaVirusi vya CoronaMjusi-kafiriViwakilishi vya idadiAdolf HitlerMohamed HusseinNduniBintiFutiYombo VitukaVita vya KageraHeshimaKarafuuShahada ya AwaliBarua pepeBarua rasmiOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaMkonoMafumbo (semi)Chuo Kikuu cha DodomaOrodha ya Marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoBahari ya HindiBogaMichael JacksonTanganyika African National UnionMbogaWhatsAppKuchaAina za manenoShangaziFasihi ya KiafrikaMalipoMwanamkeBendera ya ZanzibarFranco Luambo MakiadiMatumizi ya lugha ya KiswahiliHussein Ali MwinyiVielezi vya idadiHomoniMsamiatiUlumbiKoffi Olomide🡆 More