Usambazaji wa nguchiro (kuna spishi zaidi ambapo rangi ni nzito zaidi)
Nguchiro (Kiing.mongoose) ni wanyama wadogo kiasi wa familiaHerpestidae. Kuna spishi nne huko Madagaska ziitwazo nguchiro pia (nguchiro-bukini) na ambazo ziliainishwa katika Herpestidae, lakini malinganisho ya ADN yameonyesha kwamba spishi hizi zina mnasaba zaidi na spishi za Eupleridae. Sasa zimepewa nusufamilia yao binafsi Galidiinae. Nguchiro wa kweli wanatokea Afrika, Asia na Ulaya ya kusini. Wamewasilishwa katika visiwa kadhaa vya Karibi na Hawaii ambapo wamekuwa usumbufu.
Wanyama hawa ni warefu na wembamba na wana mkia mrefu wenye manyoya mengi. Wanafanana na chororo lakini wako wakubwa zaidi. Rangi yao ni hudhurungi, kahawia, kijivu au nyeusi. Wao ni wanyama mbua na hula wadudu, kaa, nyungunyungu, mijusi, nyoka, ndege na wagugunaji, na mara nyingi mayai na mizoga pia. Nguchiro hujulikana kwa uwezo wao wa kuua nyoka na kukinga sumu yao. Huishi peke yao au kwa makundi (k.m. nguchiro miraba na nguchiro-jangwa) na hukiakia mchana lakini pengine usiku pia.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nguchiro, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses. ®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.