Eris (alama: ; pia (136199) Eris au 136199 Eris) ni sayari kibete kubwa inayojulikana katika mfumo wa Jua letu.
Njia yake ya kuzunguka jua ni nje ya njia ya Pluto. Eros inaonekana ina angalau mwezi mmoja unaoitwa Dysnomia. Makadirio ya kipenyo chake ni 2400 km ambacho ni kikubwa kidogo kuliko Pluto. Inazunguka jua katika muda wa miaka 556.7 ya dunia. Umbali wake na jua ni mara 97 umbali wa dunia yetu. Kutoka Eris hata jua letu laonekana kama nyota ndogo tu.
Eris ilitambuliwa 2005 na wanaastronomia walioongozwa na Dr. Michael E. Brown kwenye paoneaanga Mount Palomar (Marekani). Walichungulia picha za anga zilizopigwa mwaka 2003 wakatambua nukta ya anga lililobadilika mahali.
Kutambuliwa kwa Eris kulisababisha wanafalaki kuanzisha kitengo kipya cha "sayari kibete". Brown aliwahi kutangaza Eris kuwa sayari ya kumi ya jua letu. Lakini wataalamu wengine waliona uwezekano mkubwa ya kwamba magimba mengine ya kufanana na Eris yatapatikana karibuni. Maana ya neno "sayari" kwa kulingana na sayari za ndani ilihofiwa kutavurugika. Hivyo utaratibu wa sayari kibete ulianzishwa.
Hivyo Eris ilikuwa sababu ya kushushwa kwa cheo cha Pluto ambayo ni ndogo kuliko Eris.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Eris, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.