Sofroni wa Yerusalemu (Damasko, Syria, 560 hivi - Yerusalemu, Israeli/Palestina, 11 Machi 638) alikuwa askofu wa Yerusalemu kuanzia mwaka 634 hadi kifo chake.
Wakati huo Yerusalemu ulitekwa na Waarabu Waislamu naye alitetea imani na haki za wananchi dhidi ya wavamizi.
Kabla ya hapo alikuwa mwanafunzi wa Yohane Mosko akaongozana naye kutembelea monasteri nyingi, akawa mwalimu, halafu mmonaki mwanateolojia aliyetetea vizuri imani sahihi kuhusu Yesu Kristo kuwa na utashi wa kibinadamu chini ya ule wa Kimungu.
Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Sofroni wa Yerusalemu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.