Ponsyo Pilato (kwa Kilatini Pontius Pilatus; kwa Kigiriki Πόντιος Πιλᾶτος; kwa Kiebrania פונטיוס פילאטוס; alikuwa liwali wa kiroma katika Palestina kwenye miaka 26-36.
Anajulikana kutoka vyanzo mbalimbali, lakini hasa kwa sababu ya Injili kumtaja kama hakimu aliyempeleka Yesu kuuawa msalabani. Vyanzo vingine ni katika maandiko ya Yosefu Flavius, Tacitus na Filo wa Aleksandria.
Waandishi Wayahudi Josephus na Philo wanamwonyesha kama mtawala mkali asiyeheshimu utamaduni na imani ya wenyeji wa Palestina. Baada ya kutumia unyama katika ukandamizaji wa Wasamaria aliitwa kurudi Roma na kufika mbele ya Kaisari. Hakuna habari za uhakika kuhusu maisha yake ya baadaye.
Kanisa la Ethiopia linafuata hadithi ya kwamba aliongoka, hivyo linamheshimu kama mtakatifu.
Kadiri ya mapokeo mengine, alijiua.
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ponsyo Pilato kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ponsyo Pilato, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.