Monoksidi kabonia (pia: Monoxidi ya kaboni, kwa Kiingereza carbon monoxide) ni kampaundi inayounganisha atomi moja ya oksijeni na atomi moja ya kaboni katika molekuli.
Inatokea wakati wa kuchoma kaboni, yaani mata ogania, kama kuna oksijeni kidogo tu; katika mchakato wa kawaida hutokea dioksidi kabonia.
Ni fueli nzuri inaoonyesha miale ya buluu wakati wa kuwaka. Katika hali ya gesi ni sumu kali isiyo na ladha, harufu wala rangi.
Inaweza kusababisha kifo kama moto unawaka katika nyumba au jikoni na watu wanaivuta ndani ya mapafu; inaingia katika damu na kuzuia usafirishaji wa oksijeni katika seli nyekundu za damu.
Monoksidi kabonia ina matumizi mbalimbali ya kiteknolojia, kwa mfano katika uzalishaji wa chuma kutoka mbale kwa sababu inaondoa oksijeni kwenye mbale unaoyeyushwa.
Fomula yake ni
au kwa kupuliza mvuke wa maji katika makaa ya kuwaka
Iliwahi kutumiwa kama fueli ya magari kwa kuchoma vipande vya kuni kwa joto duni na gesi iliweza kuchomwa ndani ya injini ya gari.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Monoksidi kabonia, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.