Luciano Wa Samosata

Luciano wa Samosata (takriban 125 – baada ya 180) alikuwa mhutubu na mwandishi kutoka mji wa Samosata katika Syria wakati wa Dola la Roma.

Lugha yake ya asili pengine ilikuwa Kisirya lakini kazi zake zote zilizohifadhiwa zimeandikwa kabisa kwa Kigiriki cha Kale. Mtindo wa maandiko yake ulikuwa hasa tashtiti ambamo alikejeli ushirikina na desturi za kidini.

Luciano Wa Samosata
Luciano jinsi mchoraji wa karne ya 17 alivyomwaza.

Luciano alikuwa na athari kubwa katika fasihi ya Magharibi. Kazi zilizochochewa na maandishi yake ni pamoja na Utopia ya Thomas More, kazi za François Rabelais, Timon of Athens ya William Shakespeare na Safari za Gulliver ya Jonathan Swift.

Zaidi ya kazi 80 zinazoaminiwa kuandikwa na Luciano zimehifadhiwa. Luciano alilenga hadhira ya Kigiriki iliyoelimika sana, ya tabaka la juu.

Lucian alikuwa mmoja wa waandishi wa kwanza wa riwaya katika ustaarabu wa magharibi. Hadithi ya Kweli ( Ἀληθῆ διηγήματα ) ilikuwa kazi ya masimulizi ya kubuni. Katika hadithi hii aliiga baadhi ya hadithi za ajabu zilizosimuliwa na Homer katika Odisei na pia habari zilizorekodiwa na mwanahistoria Thucydides . Alitarajia mandhari ya kisasa bunilizi ya kisayansi ikiwa ni pamoja na safari za kwenda mwezini na hadi Zuhura, uhai wa nje na vita kati ya sayari. Riwaya hiyo mara nyingi huchukuliwa kuwa kazi ya kwanza inayojulikana ya bunilizi ya kisayansi.

Matoleo

Marejeo

Viungo vya nje

Tags:

125180Dola la RomaKiyunaniMwandishiSyriaTashtitiUshirikina

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Kima (mnyama)Orodha ya viwanja vya ndege nchini TanzaniaUkooHistoria ya KiswahiliBunge la Afrika MasharikiAfrika KusiniJuaMbuniMawasilianoDNAWamasaiMpwaSalaTarafaTarakilishiMajira ya mvuaAfrikaKaabaKishazi tegemeziKiini cha atomuMongoliaNgiriKamusi Hai ya Kiswahili MtandaoniKylian MbappéPasifikiKilimoBaruaSerikaliJomo KenyattaMuzikiMfumo katika sokaBoris JohnsonBenderaMasharikiSayariWiktionaryBibliaUshogaDodoma (mji)KisononoHistoria ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoUundaji wa manenoAmri KumiVasco da GamaLionel MessiHistoria ya EthiopiaMbossoAir TanzaniaNomino za dhahaniaSheriaKaramu ya mwishoJumuiya ya Afrika MasharikiGesi asiliaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaUgaidiEkaristiMkoa wa RuvumaNyaniPalestinaLeopold II wa UbelgijiSanaaKamusi ya Kiswahili sanifuOrodha ya Marais wa ZanzibarJumaUajemiSenegalKoffi OlomideOrodha ya makabila ya TanzaniaViwanja vya Afrika (Kwa Ukubwa)Soko la watumwaVieleziUhifadhi wa fasihi simuliziUsultani wa ZanzibarMamba (mnyama)Real Betis🡆 More