Jumba la makumbusho la Karen Blixen ni jina linalotumiwa kwa majumba ya makumbusho mawili; moja la Denmark, na lingine nchini Kenya.
.
Jumba la makumbusho la Karen Blixen huko Denmark liko katika mji wa Rungstedlund, nyumba ya mwandishi Karen Blixen (1885-1962), katika mji wa Rungsted, Denmark (takribani km 24 kaskazini mwa Kopenhagen). Alitumia muda mwingi wa maisha yake nchini Kenya barani Afrika na mwaka 1937 aliandika kitabu Out of Afrika. Jumba hili la makumbusho linajumuisha vitabu vingi kutoka maktaba yake Karen Blixen na pia idadi ya picha za Kiafrika alizochora.
Karen Blixen aliishi wingi wa maisha yake katika familia iliyokuwa na mali isiyohamishika mjini Rungstedlund, ambayo ilikuwa inamilikiwa na baba yake mwaka wa 1879, kaskazini mwa Copenhagen (mji mkuu wa Denmark). Maeneo haya Kongwe yamekuwa tangu mwaka wa 1680, na ingeli ziliendeshwa zote kama hoteli na kama shamba. Kuandika kwingi kwa Blixen kulifanyika katika chumba chake cha Ewald, lililopata jina hilo kutoka kwa mwandishi Johannes Ewald. Mali hiyo inasimamiwa na Rungstedlund Foundation, iliyoanzishwa na Blixen na ndugu zake. Mali hiyo ilifunguliwa kwa umma kama jumba la makumbusho mwaka wa 1991.
Jumba la makumbusho la Rungstedlund ni mojawapo ya majumba ya makumbusho ya kwanza ya Kideni ambayo imetabarukiwa tovuti.
Rungstedlund ramani inaratibu: 55 º 53.000 'N na 12 º 32.600' E.
Jumba la makumbusho la Karen Blixen barani Afrika iko karibu na Nairobi, Kenya, na lilikuwa nyumbani kwake "Mbogani" kati ya miaka 1917 na 1931, wakati huo katikati ya mashamba makubwa ya kahawa kutokana na takriban Ha 2000 (ekari 5000). Ilichangiwa na serikali ya Kideni na kufunguliwa mwaka wa 1986, kufuatia umaarufu wa filamu wa mwaka wa 1985, Out of Africa. Sikuhizi jumba hilo la makumbusho liko katika kitongoji cha Karen na ni vigumu wewe kupata kahawa pale, lakini kuna nyumba za kitajiri na farasi wengi.
Jumba hilo la makumbusho haukutumika kwa ajili ya filamu ya Out of Africa kwani picha zilichukuliwa katika nyumba yake ya kwanza, Mbagathi,hapo jirani, ambako aliishi kati ya mwaka 1914 na 1917.
Ramani ya majumba ya makumbusho ya Kenya inaratibu: 1 º 21.110 'S na 36 º 42.750' E.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jumba la makumbusho la Karen Blixen, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.