Waraka wa pili wa Yohane ni kitabu kifupi kuliko vyote 27 vya Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Kuanzia karne ya 5 mapokeo yamemtaja Mtume Yohane kuwa mwandishi wa barua hii, kwa sababu yaliyomo, misamiati na mtindo wa mawazo vinalingana na vile vya Waraka wa kwanza wa Yohane. Lakini barua yenyewe inamtaja tu "mzee" kuwa mwandishi wake.
Sawa na maandishi mengine ya jumuia za Yohane, barua hiyo inafikiriwa kuandikwa mwishoni mwa karne ya 1 huko Efeso ili kuangalisha dhidi ya wazushi. Katika barua hii linaonekana kwa mara ya kwanza jina la "Mpingakristo".
Makala hii kuhusu mambo ya Agano Jipya bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Waraka wa pili wa Yohane kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Waraka wa pili wa Yohane, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.