Ushirika kamili ni msamiati wa teolojia ya Ukristo kuhusu Kanisa.
Unamaanisha umoja kamili kati ya madhehebu mbalimbali kwa msingi wa imani ileile inayoyawezesha kushirikiana kikamilifu katika ibada na hasa ekaristi na sakramenti nyingine.
Unatumika na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa mashariki, ukitofautishwa na ushirika usio kamili au wa kiasi tofautitofauti uliopo kati ya Wakristo wa aina zote kadiri wanavyozidi kusadiki mambo yaleyale ya msingi zaidi (kama vile Utatu mtakatifu, umungu wa Yesu Kristo na ufufuko wake), ingawa wanapishana katika mengine (hasa Kanisa na sakramenti).
Dhana ya ushirika kamili hutumiwa pia kutaja uhusiano baina ya makanisa ya Jumuiya Anglikana na pia kati ya makanisa mengine ya Kiprotestanti ambayo yameamua kutambuana na kushirikiana moja kwa moja.
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ushirika kamili kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ushirika kamili, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.