Larus Linnaeus, 1758 Pagophila Kaup, 1829 Rissa Stephens, 1826 Rhodostethia MacGillivray, 1842 Xema Leach, 1819
Shakwe | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Shakwe kichwa-kijivu | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
|
Shakwe ni ndege wa familia Laridae. Watu wengi huita spishi za Sternidae shakwe pia. Spishi za Laridae zina michanganyiko ya rangi nyeupe, nyeusi na ya kijivu; nyingine ni nyeupe kabisa, nyingine kijivucheusi. Ndege hao wana domo lenye nguvu na ncha kali; domo lao ni nene kuliko lile la spishi za Sternidae. Wanaweza kuogelea na wana ngozi kati ya vidole vyao.
Shakwe huhusiswha na pwani, na kweli huko wako tele, lakini spishi nyingi wanatokea mbali na bahari, kwa kawaida karibu na maji. Spishi za Rissa huonekana baharini mbali na pwani. Shakwe huwakamata samaki wadogo au kaa au gegereka wengine lakini hula mizoga pia. Hulitengeneza tago lao chini, mara nyingi kisiwani.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Shakwe, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.