Papa Gregori Xiii

Papa Gregori XIII (Bologna, Italia, 7 Januari 1502; Roma, 10 Aprili 1585) alikuwa Papa wa Kanisa Katoliki kuanzia tarehe 13/25 Mei 1572 hadi kifo chake.

Alitokea Bologna, Italia.

Papa Gregori Xiii
Papa Gregori XIII.

Alimfuata Papa Pius V akafuatwa na Papa Sixtus V.

Anakumbukwa hasa kwa matengenezo ya kalenda iliyokuja kujulikana kama "kalenda ya Gregori" ikawa kalenda ya kimataifa kote duniani hadi leo.

Maisha

Alizaliwa kwa jina la Ugo Buoncampagni akafuata masomo ya sheria na kuwa profesa wa sheria kwenye chuo kikuu cha Bologna.

Mwaka 1539 aliitwa na Papa Paulo III akapewa kazi mbalimbali kama mwanasheria wa Kanisa.

Baadaye Papa Paulo IV alimpa cheo cha askofu wa Viesti (Italia) na ni hapo tu kwamba Ugo alikula kiapo cha upadri na kuwekwa wakfu kama askofu moja kwa moja.

Baada ya kifo cha Papa Pius V alichaguliwa kuwa mwandamizi wake, akachukua jina la "Gregorius".

Papa Gregori XIII alijitahidi kurudisha nyuma mwendo wa matengenezo ya Kiprotestanti. Alikubali dhuluma dhidi ya Wakristo wa Kiinjili nchini Ufaransa tarehe 23 - 24 Agosti 1572 ("Usiku wa Bartolomeo").

Alijaribu kukusanya mataifa ya Ulaya dhidi ya Dola la Uturuki kwa shabaha ya kukomboa mji wa Konstantinopoli lakini hakufaulu.

Pamoja na jitihada hizi za kisiasa alijenga taasisi ya taaluma. Aliunda Chuo Kikuu cha Kipapa huko Roma kinachoitwa kwa heshima yake "Gregoriana" hadi leo.

Kalenda mpya hakuitunga mwenyewe, lakini aliita wataalamu katika kamati maalumu na kukubali mapendekezo waliyotoa tarehe 24 Februari 1582.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Papa Gregori Xiii  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Gregori XIII kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.

Tags:

Papa Gregori Xiii MaishaPapa Gregori Xiii Tazama piaPapa Gregori Xiii TanbihiPapa Gregori Xiii Viungo vya njePapa Gregori Xiii10 Aprili13 Mei15021572158525 Mei7 JanuariBolognaItaliaKanisa KatolikiKifoPapaRomaTarehe

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Tendo la ndoaHistoria ya IranHistoria ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoHistoria ya WapareHistoria ya AfrikaUkooKiazi cha kizunguVichekeshoBiasharaMahindiMbadili jinsiaRushwaLady Jay DeeTafsiriKoroshoJay MelodySah'lomonLongitudoJeshi la Ulinzi la Wananchi wa TanzaniaHadithiRedioMafurikoOrodha ya majimbo ya MarekaniUchumiChama cha MapinduziMbwana SamattaAmina ChifupaNomino za dhahaniaWizara za Serikali ya TanzaniaUpinde wa mvuaIsraeli ya KaleWema SepetuKilimoWilaya ya IlalaMishipa ya damuNusuirabuMillard AyoHistoria ya UislamuUmoja wa MataifaWasukumaUchaguzi Mkuu wa Tanzania, 2020HomoniVivumishi vya pekeeSerikaliUbungoUchawiMajiTiktokMkoa wa Dar es SalaamEe Mungu Nguvu YetuHarmonizeMaana ya maishaWarakaKigoma-UjijiKanisa KatolikiUenezi wa KiswahiliTanganyika African National UnionAlizetiSheriaLigi Kuu Tanzania BaraKomaTanzaniaWilaya ya ArushaAntibiotikiVidonda vya tumboSarufiVielezi vya idadiTupac ShakurVipera vya semiMimba kuharibika🡆 More