Omar Chayyām (Kifarsi: عمر خیام ’omar-e khayyām ; * mnamo 1048 mjini Nishapur, mkoa wa Khorasan; † kati ya 1122 - 1131) alikuwa mshairi nchini Uajemi aliyejulikana pia kama mtaalamu wa hisabati, falaki na falsafa.
Kama mwanahisabati aligundua usuluhisho wa milingano ya mchemraba pamoja na kipeo cha mchemraba. Mfalme alimwagiza 1073 kujenga jengo la kuangalia nyota. Akaendelea kutunga kalenda iliykuwa msingi wa kalenda ya jua ya Uajemi inayotumiwa hadi leo na kalenda hii imesifiwa kuwa kamili kushinda kalenda ya Gregori.
Alitunga mashairi aina ya rubaiyat yaliyokuwa na mistari minne kila beti akatunga zaidi ya 1,000. Katika mashairi haya alijadili mawazo yake juu ya falsafa na dini ya Kiislamu.
Alikuwa na elimu nzuri lakini hakupendezwa na Uislamu wa kawaida wa wakati wake. Kati ya mabeti mashuhuri aliyotunga ni
"Furahia divai na wanawake usiogope maana Allah ni mwenye rehema."
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Omar Khayyam kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Omar Khayyam, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.