Neopalpa donaldtrumpi ni spishi ya nondo iliyogunduliwa mwaka 2017 na mtaalamu wa Kanada Vazrick Nazari.
Neopalpa donaldtrumpi | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kichwa cha Neopalpa donaldtrumpi kwa kuitazama kutoka upande wa kushoto na mbele. | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Akiwa mgunduzi wa spishi mpya Nazari aliweza kuchagua jina akaamua kutumia jina la mwanabiashara na wakati ule mgombea wa uraisi Donald Trump kwa matumaini ya kwamba chaguo hili litasababisha watu wengi zaidi kusikia habari za wadudu na utafiti wa wadudu.
Jenasi Neopalpa pamoja na spishi Neopalpa neonata ilielezwa mara ya kwanza mwaka 1998 na Dalibor Povolný. Miaka 20 baadaye Vazrick Nazari aliangalia upya mifano ya kipepeo hiki iliyohifadhiwa katika taasisi ya Bohart Museum of Entomology. Alitambua ya kwamba mifano kadhaa ilitofautiana na mingine na kuwa spishi mpya aliyoiita Neopalpa donaldtrumpi kwa sababu ya vigamba vya rangi ya njano-nyeupe kichwani. Haya yalimkumbusha kuhusu nywele za Donald Trump. Ilhali nafasi yake ya kueleza spishi mpya ilitokea karibu na tarehe ya Trump kuingia katika uraisi kwenye januari 2017 aliamua kutumia hili kwa sababu aliona sayansi ya wadudu ilihitaji kujulikana zaidi.
Mwili wa kipepeo hiki una urefu baina ya milimita 7 na 13. Mabawa yake hufunika upana wa milimita 6 hadi 9.2. Uso wa juu wa mabawa huwa na rangi kahawia pamoja na madoa meupe zaidi. Kichwa kina vigamba vyeupe-njano yaliyosababisha uteuzi wa jina. Pamoja na vigamba vya kichwani tofauti nyingine ya spishi hii na spishi ya N. neonata ni udogo wa mboo na pia umbo la sehemu za kike. Zinatofautishwa pia kutokana na DNA.
Hadi sasa Neopalpa donaldtrumpi ilionekana kwenye sehemu za kaskazini ya rasi ya Baja California katika Meksiko na kwenye kaskazini ya Kalifornia ya Marekani.
Wikispecies has information related to: Neopalpa donaldtrumpi |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Neopalpa donaldtrumpi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.