Nawal El Saadawi (kwa Kiarabu: نوال السعداوي ; O 4 Oktoba 1931 – 21 Machi 2021) alikuwa mwandishi wa habari, mwanaharakati aliyetetea haki za wanawake, daktari na mtaalamu wa magonjwa ya akili kutoka Misri.
Aliandika vitabu vingi juu ya mada ya wanawake katika Uislamu, akizingatia sana mila ya ukeketaji katika jamii yake. Alielezewa kama "mwandishi na mtetezi wa Ulimwengu wa Kiarabu", na kama "mwanamke mkali zaidi wa Misri". Alikuwa mwanzilishi na rais wa Jumuiya ya Mshikamano wa Wanawake wa Kiarabu na mwanzilishi mwenza wa Jumuiya ya Waarabu ya Haki za Kibinadamu.
Alitunukiwa digrii za heshima katika mabara matatu. Mnamo 2004 alishinda Tuzo ya Kaskazini-Kusini kutoka Baraza la Uropa. Mnamo mwaka 2005 alishinda Tuzo ya Kimataifa ya Inana nchini Ubelgiji, na mwaka wa 2012 Ofisi ya Kimataifa ya Amani ilimtunuku Tuzo ya Amani ya Seán MacBride ya mwaka 2012.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nawal El Saadawi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.