Ubepari

Ubepari ni mfumo wa uchumi ambamo biashara, viwanda na vitegauchumi vingine vinatawaliwa na watu binafsi kwa kiasi kikubwa na kwa lengo la kupata faida.

Nafasi ya serikali ni ndogo. Vilevile lengo la kuhudumia jamii katika mahitaji yake haliongozi mipango.

Ubepari
Injini kama hii, iliyotegemea makaa, ilisukuma mapinduzi ya viwanda huko Britania.
Ubepari
Tangazo la ubora wa ubepari.
Ubepari
Soko la hisa la New York, Marekani (1963).

Kati ya sifa za ubepari kuna ulimbikizaji wa mtaji, ushindani katika soko huria na kazi zinazolipwa mshahara.

Katika mfumo huo, pande zinazokabiliana zinapanga zenyewe bei kwa makubaliano, bila kuingiliwa na mamlaka yoyote ya nje.

Ubepari una viwango tofauti vya uhuru huo, kadiri ya nchi:Kiingereza kinaainisha laissez-faire capitalism, welfare capitalism, crony capitalism na state capitalism.

Historia

Kihistoria, ubepari uliwahi kuwepo tangu zamani kwa namna mbalimbali, lakini ulianza kutawala baada ya mifumo ya Karne za Kati za Ulaya kupitwa na wakati na mapinduzi ya viwanda kushika kasi. Ubeberu, ukoloni, halafu utandawazi vimefanya ubepari uenee duniani kote.

Katika karne ya 20 ubepari ulishindana na mfumo mbadala wa ukomunisti ambao ulitia mkazo juu ya majukumu ya serikali katika uchumi mpaka kuwanyima wananchi nafasi ya kuwajibika. Hata hivyo, baada ya kushinda, ubepari pia umeingiza uchumi wa dunia katika hali tete, kama ilivyojitokeza mwanzoni mwa karne ya 21.

Watetezi wa ubepari wanasisitiza kwamba mfumo huo unaleta ustawi wa jamii ulio mkubwa kuliko ule unaoletwa na mifumo mingine yoyote, kiasi kwamba hatimaye wote wanafaidika, si matajiri tu. Critics of capitalism variously associate it with economic instability,

Wengi wanapinga hoja hiyo kwa kuonyesha umati unaokosa kazi na huduma za msingi kutokana na pesa kutiwa maanani kuliko binadamu na mazingira kutumika kuliko uwezo wake wa kustahimili.. Kanisa Katoliki limejitokeza kwa namna ya pekee kati ya dini mbalimbali kukosoa ubepari kama ulivyokosoa na hatimaye kuangusha ukomunisti wa Ulaya Mashariki (1989) likiongozwa na Papa Yohane Paulo II.

Tanbihi

Marejeo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Ubepari 
Wiki Commons ina media kuhusu:
Ubepari  Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ubepari kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

Ubepari HistoriaUbepari TanbihiUbepari MarejeoUbepari Marejeo mengineUbepari Viungo vya njeUbepariBiasharaFaidaJamiiSerikaliViwanda

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Agano JipyaMaadiliTafsiriKifua kikuuUwanja wa Taifa (Tanzania)MeliMahindiMaudhuiSkeliVivumishi vya pekeeBibliaNgw'anamalundiNg'ombePepopundaShahawaNabii EliyaBiashara ya watumwaUkoloni MamboleoUbatizoSimbaVivumishi vya urejeshiShikamooInsha ya wasifuYouTubeKaabaMizimuMwakaKonsonantiKylian MbappéMobutu Sese SekoUtoaji mimbaSilabiNamba ya mnyamaJokate MwegeloTaswira katika fasihiVatikaniMbossoLenziUhifadhi wa fasihi simuliziMartin LutherDhanaWordPressMnyamaMavaziNetiboliSarufiViwakilishi vya urejeshiMnyoo-matumbo MkubwaFonimuNimoniaUgonjwa wa kuharaUharibifu wa mazingiraElizabeth MichaelUmaskiniUbongoMjasiriamaliMkoa wa MwanzaKiunguliaJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaKamusi Hai ya Kiswahili MtandaoniMarekaniMeridianiMtandao wa kompyutaMbuMaajabu ya duniaKiswahiliMafumbo (semi)Nomino za dhahaniaMuhammadJipuHarmonizeKipindupinduInsha za hojaVitendawiliHoma ya iniLahajaNdoaImani🡆 More