Mnyama Lama

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Lama
Lama anayelala (Lama glama)
Lama anayelala
(Lama glama)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Tylopoda (Wanyama wenye miguu inayovimba)
Familia: Camelidae (Wanyama walio na mnasaba na ngamia)
J. E. Gray, 1821
Jenasi: Lama (Lama na Guanako)
Cuvier, 1800
Spishi: L. glama (Lama)
(Linnaeus, 1758)
Usambazaji wa lama na vikunya
Usambazaji wa lama na vikunya

Lama ni mnyama wa kufugwa wa spishi Lama glama katika familia Camelidae, anayeishi Amerika Kusini. Lama ametumiwa kwa upana na watu wa milima ya Andes tangu kabla ya historia, kwa nyama yake na kubeba mizigo.

Maelezo

Mnyama Lama 
Lama wa kufugwa

Lama mzima ana kimo cha mita 1.7–1.8 juu ya kichwa, na uzito wa kilo 130–200. Wakati wa kuzaliwa, lama mchanga ana uzito wa kilo 9 hadi 14. Kwa kawaida, lama wanaishi miaka 15–25, na lama wengine wamejulikana kuishi zaidi ya miaka 30.

Mnyama Lama 
Jika na ndama wake

Lama ndio wanyama wa kijamii sana, na huishi pamoja katika makundi. Sufu ya lama ni laini sana na haina lanolini. Lama wana akili na huweza kufundishwa kazi rahisi baada ya kuzirudia mara chache. Wakitumia tandiko la mzigo, wanaweza kubeba takribani asilimia 25–30 ya uzito wa mwili wao kwa safari ya km 8–13.

Jina la lama lilitokea jina la Kingereza "llama", lililochukuliwa toka lugha ya wenyeji wa Peru.

Inaonekana kwamba lama wamekuja kwa asili kutoka nyanda za Amerika Kaskazini takribani miaka milioni 40 iliyopita. Walihamia Amerika Kusini takribani miaka milioni tatu iliyopita. Mwishoni mwa zama ya barafu ya mwisho (miaka 10,000–12,000 iliyopita), wanyama wa familia Camelidae walikuwa wametoweka Amerika Kaskazini. Mnamo 2007, idadi ya lama na alpaka pamoja ilikuwa zaidi ya milioni saba Amerika Kusini, na kutokana na uingizaji kutoka Amerika Kusini mwishoni mwa karne ya 20, sasa kuna zaidi ya lama 158,000 na alpaka 100,000 wanaoishi Marekani na Kanada.

Marejeo

Mnyama Lama 
Wiki Commons ina media kuhusu:

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wiki: WikiProject Mammals/Article templates/doc.

Tags:

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Saida KaroliOrodha ya vyama vya siasa TanzaniaDhamiriKataKutoka (Biblia)Wiki FoundationJuxUkristo barani AfrikaJacob StephenOrodha ya shule nchini TanzaniaMisriTaasisi ya Taaluma za KiswahiliSiasaChuraVivumishi vya sifaInsha ya wasifuMunguSentensiJokate MwegeloUkomboziUbakajiWanyamweziChombo cha usafiri kwenye majiUsawa (hisabati)YouTubeKupatwa kwa MweziWahayaWilliam RutoHekaya za AbunuwasiWalawi (Biblia)Vivumishi vya idadiBiashara ya watumwaMkoa wa Dar es SalaamTaasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya TanzaniaBarabaraNamba ya mnyamaSayariUti wa mgongoWilaya za TanzaniaVielezi vya mahaliNg'ombeShairiMtaalaOrodha ya wanamuziki wa AfrikaKinembe (anatomia)UlayaUkristoMike TysonOrodha ya vyama vya kisiasa nchini KenyaMkoa wa MtwaraVitendawiliWimbo wa Jumuiya ya Afrika MasharikiSaharaAlomofuOrodha ya viwanja vya ndege nchini TanzaniaKamusi Hai ya Kiswahili MtandaoniMkoa wa SingidaHassan bin OmariSilabiKadi ya adhabuJumamosi kuuBabeliDaudi (Biblia)UyahudiUchimbaji wa madini nchini TanzaniaAir TanzaniaMashuke (kundinyota)ZuchuDuma🡆 More