P.
Koho | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Koho aliyekamata samaki | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
|
Koho ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Pandion, jenasi pekee ya familia Pandionidae. Zamani spishi moja tu ilifahamiwa, lakini bingwa kadhaa wamekupa nususpishi ya Australasia cheo cha spishi sasa na IOC (Muungano wa Kimataifa wa Wataalamu wa Ndege) unaiafiki. Lakini wataalamu wengine hawakubali.
Mwili wa koho ana sm 50-66 na upana wa mabawa ni sm 127-180. Mgongo wake una rangi ya kahawa na kidari na tumbo ni nyeupe. Mara nyingi kidari kina michirizi kahawia. Kichwa ni cheupe chenye kinyago. Vidole vyote vina urefu sawa na vina kucha za mviringo bila mfuo kinyume na vipanga na jamaa. Kidole cha nje kinaweza kugeuzwa kuelekea nyuma, kiasi kwamba koho anaweza kushika mawindo kwa vidole viwile mbele na viwili nyuma. Hii inafaa hasa akikamata samaki wenye kuteleza. Koho hula samaki takriban pekee, lakini pengine hukamata wagugunaji, amfibia, watambaazi na ndege wengine. Hutengeneza tago lao kwa vijiti juu ya mti, mhimili ya huduma za umma au mwamba. Jike huyataga mayai 2-4.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Koho, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.