Jangwa Kubwa la Victoria (Great Victoria Desert) ni jangwa kubwa zaidi nchini Australia.
Linaenea kwa km² 348,750 katika kusini magharibi ya bara hili. Uso wake ni mchanganyiko wa matuta ya mchanga, vilima vidogo, tambarare za nyasi, maeneo makubwa ya changarawe, na maziwa ya chumvi.
Jangwa hilo linapatikana katika majimbo ya Australia Magharibi na Australia Kusini. Urefu wake kutoka mashariki hadi magharibi ni kama km 700.
Tabianchi ni yabisi sana, usimbishaji wa mwaka ni kati ya milimita 200 hadi 250 za mvua kila mwaka.
Lilipewa jina lake kwa heshima ya Malkia Victoria wa Uingereza.
Wakazi asili wa Australia bado wanaishi katika sehemu ya jangwa wanapokalia eneo kubwa la kujitawala.
Makala hii kuhusu maeneo ya Australia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Jangwa Kubwa la Victoria kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jangwa Kubwa la Victoria, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.