Eneo la vijijini (kwa Kiingereza: rural area, countryside) ni eneo ambalo si mji wala jiji.
Mara nyingi ni eneo la kilimo au mashamba. Kwa hiyo watu husema pia "mashambani". Wakazi wake wanaoishi humo hukaa katika vitongoji au vijiji; wakati mwingine pia sehemu pasipo nyumba nyingine.
Kwa kawaida maeneo ya vijijini hakuna msongamano mkubwa wa watu na makazi hayana nyumba nyingi kama mji.
Vijijini ni kinyume cha neno "mjini" linalomaanisha eneo ambako majengo ni mengi na watu wengi hukaa pamoja.
Nchi nyingi zinafafanua "maeneo ya vijijini" kwa matumizi ya kitakwimu lakini fafanuzi hizi zinatofautiana.
Kisheria kuna tofauti kati ya maeneo ya mjini (urban) na vijijini (rural) kwenye nchi tofauti kuhusu kiwango cha madaraka ya kujitawala, kiasi cha fedha kinachopangiwa kwa matumizi ya serikali, ubora wa miundombinu, huduma na kadhalika. Mara nyingi vijijini umaskini ni mkubwa kuliko mjini.
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Eneo la vijijini kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Eneo la vijijini, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.