Dennis Brutus (28 Novemba 1924 - 26 Desemba 2009) alikuwa mwandishi wa Afrika Kusini.
Kwa vile aliandika dhidi ya ubaguzi wa rangi alifungwa jela na baadaye kuishi uhamishoni 1966-1990. Hasa alitunga mashairi na alifundisha kama profesa wa ushairi nchini Marekani.
Dennis Brutus alizaliwa tarehe 28 Novemba, mwaka wa 1924 mjini Salisbury, Rhodesia, ambapo sasa huitwa Harare nchini Zimbabwe. Alisomewa kwenye Paterson High School nchini Afrika Kusini na kupata ushahada wake wa kwanza kutoka Chuo Kikuu cha Fort Hare katika somo la Kiingereza mwaka wa 1947. Mwaka wa 1950 alimwoa May Jaggers, wakawa na watoto wanane. Kuanzia 1948 hadi 1961, Brutus alifundisha Kiingereza na Kiafrikaans kama mwalimu wa sekondari mjini Port Elizabeth. Mwaka wa 1960 alianza pia kufanya kazi kama mwandishi wa habari. Kwa vile aliandika dhidi ya siasa ya apartheid, alifungwa jela kisiwani mwa Robben kwa miezi 18 (1964-65), na kutoka Afrika Kusini mwaka wa 1966. Uhamishoni kwanza alifanya kazi mjini London kwa shirika la International Defence and Aid Fund. Mwaka wa 1971 akahamia Marekani. Kule akawa profesa wa chuoni, kwanza kwa somo la Kiingereza katika Chuo Kikuu cha Northwestern mjini Evanston (1971-85), na hatimaye tangu mwaka wa 1986 akawa profesa katika idara ya elimu ya kijamii ya watu weusi, Chuo Kikuu cha Pittsburgh.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Dennis Brutus, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.