Bakteriolojia

Bakteriolojia ni tawi la biolojia linalochunguza bakteria.

Ni sehemu ya mikrobiolojia.

Bakteriolojia
Antonie van Leeuwenhoek, mwanamikrobiolojia wa kwanza na mtu wa kwanza aliyeona bakteria kwa darubini.

Historia

Bakteria waligunduliwa mara ya kwanza na Antonie van Leeuwenhoek mwaka 1676, kwa kutumia hadubini ya lensi moja ya muundo wake mwenyewe. Aliwaita "animalcules" na alichapisha habari za utafiti wake kwenye msururu wa barua kwa Shirika la Muungano wa Mfalme.

Jina bacteriam lililetwa miaka mingi baadaye, na Christian Gottfried Ehrenberg katika mwaka 1838.

Mwaka 1859 Louis Pasteur alionyesha kuwa mchakato wa kuchachusha unasababishwa na ukuaji wa vijiumbe, na kwamba ukuaji huo si wa kizazi cha kujianzia. (Hamira na kuvu, ambazo kwa kawaida zinahusishwa na uchachushaji, si bakteria, ila ukungu.) Pamoja na mwenzake, Robert Koch, Pasteur alikuwa wa kwanza kuitetea nadharia ya kijidudu kisababishi cha ugonjwa.

Robert Koch alikuwa mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi wa mikrobiolojia na alishughulikia kipindupindu, kimeta na kifua kikuu. Katika utafiti wake wa kifua kikuu, Koch hatimaye alithibitisha nadharia ya kijidudu, ambayo ilimfanya atunukiwe Tuzo la Nobel mwaka 1905. Katika madai yake, Koch aliweka vigezo vya kutathmini kama kiumbehai ndiye husababisha ugonjwa, na madai hayo yanatumika mpaka leo hii.

Ingawa katika karne ya 19 ilijulikana kwamba bakteria ndio chanzo cha magonjwa mengi, hakuna matibabu yoyote ya viuabakteria yaliyopatikana. Katika mwaka 1910, Paul Ehrlich alitengeneza kiuavijasumu cha kwanza, kwa kubadilisha rangi ambazo kwa kuchagua zilitia mawaa Treponema pallidum, spirokaeti ambayo husababisha kaswende katika mchanganyiko ambao uliua kisababishi magonjwa. Ehrlich alikuwa ametuzwa Tuzo la Nobel mwaka 1908 kwa kazi yake kuhusu elimu ya kingamaradhi, na alianzisha matumizi ya madoa ili kuchunguza na kubaini bakteria, na kazi yake ilijikita kwenye misingi ya doa la Gram na doa la Ziehl-Neelsen.

Mafanikio makubwa katika utafiti wa bakteria yalikuwa kutambuliwa kwa Carl Woese mwaka 1977 kwamba akea walitokana na mabadiliko tofauti na yale ya bakteria. Uanishaji huo mpya wa jamii ya filojenetikia ulikitwa kwenye misingi ya kufululizwa kwa ribosomu RNA 16S, ukagawa prokaryota katika makundi mawili yenye mageuko tofauti, kama mojawapo ya sehemu ya mifumo ya domeni tatu.

Tanbihi

Bakteriolojia  Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bakteriolojia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

BakteriaBiolojiaMikrobiolojiaTawi

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Mkoa wa KigomaMkoa wa TaboraAbedi Amani KarumeJamhuri ya Watu wa ZanzibarNamba za simu TanzaniaWilaya ya Nzega VijijiniWabunge wa Tanzania 2020JinsiaKiswahiliP. FunkWameru (Tanzania)UlimwenguKonsonantiHaki za wanyamaMivighaHekalu la YerusalemuPumuAnwaniKitenzi kikuuNamba tasaUmememajiMapambano ya uhuru TanganyikaUmoja wa MataifaKhadija KopaMaambukizi nyemeleziIsraeli ya KaleSteven KanumbaWingu (mtandao)Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, 2020Afrika KusiniMartha MwaipajaNguruwe-kayaFalsafaNomino za pekeeMbossoUvimbe wa sikioKoloniMauaji ya kimbari ya RwandaUchumiUjimaMamaHoma ya mafuaKiunguliaBikiraMuda sanifu wa duniaAlomofuKanga (ndege)Tenzi tatu za kaleSimba S.C.Bendera ya KenyaManchester CityUundaji wa manenoLionel MessiNyotaWikipediaAlama ya uakifishajiUandishi wa inshaMkoa wa Dar es SalaamMapinduzi ya ZanzibarVirusi vya CoronaFisiMisimu (lugha)Ala ya muzikiSitiariKataFani (fasihi)Vivumishi vya idadiKimeng'enyaUandishi wa barua ya simuYesuKanisa Katoliki🡆 More