Nargis Dutt (jina la kuzaliwa: Fatima Rashid lakini alifahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Nargis; kwa Kihindi: नर्गिस, kwa Kiurdu: |نرگس J: 1 Juni 1929 – 3 Mei 1981) alikuwa mwigizaji wa filamu kutoka India.
Huhesabiwa kama mmoja kati ya waigizaji filamu bora katika historia ya sinema za Kihindi.
Nargis | |
---|---|
Amezaliwa | Fatima Rashid 1 Juni 1929 Calcutta, West Bengal, Uhindi ya Kiingereza |
Amekufa | 3 Mei 1981 (umri 51) |
Kazi yake | Mwigizaji |
Miaka ya kazi | 1935, 1942 – 1967 |
Ndoa | Sunil Dutt (1958 – 1981) (mpaka kifo chake) |
Watoto | Sanjay Dutt Anju Priya Dutt |
Alipata kuonekana kwa mara ya kwanza akiwa kama mtoto kwenye seti ya Talash-E-Haq mnamo 1935, lakini kazi yake ya uigizaji ilianza rasmi 1942 na Tamanna. Wakati wa kazi zake ambazo zilitamba sana kunako miaka ya 1940 na 60, Nargis amepata kuonekana katika kazi kadhaa zenye-mafanikio, vilevile kwenye kazi ambazo ziliheshimika vibaya mno, nyingi katika hizo humshirikisha mwigizaji mwenzi na mtengenzaji wa filamu Raj Kapoor. Moja kati ya nyusika maarufu alizocheza ni pamoja na Radha (-liopa kushindanishwa kwenye Academy Award)- Mother India (1957), kazi ambayo alijipatia tuzo ya kama mwigizaji bora na Filmfare Awards na Karlovy Vary International Film Festival. Mnamo 1958, Nargis ameolewa na mshiriki mwenzake wa katika filamu ya Mother India, mwigizaji Sunil Dutt, na akaachana na masuala ya soko la filamu. Alionekana mara kadhaa tu kwenye filamu za miaka ya 60.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nargis, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.