Nagasaki ni mji wa Japani kwenye kisiwa cha Kyushu mwenye wakazi 450,000.
Umejulikana kimataifa kwa sababu uliharibiwa tarehe 9 Agosti 1945 na bomu la nyuklia la Kimarekani kama mji wa pili katika historia baada ya Hiroshima. Bomu hilo liliua watu 36,000 mara moja na wengine waliokadiriwa kuwa kati ya 70,000 na 100,000 walikufa baadaye kufuatana athari ya mnururisho wa kinyuklia.
Kihistoria Nagasaki ilikuwa kitovu cha Ukristo katika Japani mnamo mwaka 1600. Imani hiyo ilipigwa marufuku na serikali, hivyo Wakristo wengi waliuawa katika miaka iliyofuata. Wachache walitunza imani kwa siri hadi kurudishwa kwa uhuru wa dini katika karne ya 19.
Makala hii kuhusu maeneo ya Japani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Nagasaki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nagasaki, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.