Karoo (pia Karroo tamka Karu) ni eneo la nusu jangwa katika nyanda za juu za Afrika Kusini.
Inaenea kaskazini mwa mtelemko mkubwa ambako nyanda za juu zinaanza na kusini mwa Namibia. Hapa Karoo Ndogo, Karoo Kubwa na Karoo ya Juu zinatofautishwa pamoja na Karoo ya Sukulenti na Karoo ya Wanama. Ikiwa na eneo la kilomita 500,000 za mraba, Karoo inajumuisha karibu theluthi moja ya eneo la Afrika Kusini.
Hakuna ufafanuzi kamili wa Karoo kwa hiyo hakuna mipaka maalumu. Mfafanuzi hutegemea uso wa nchi, jiolojia, tabianchi na hasa kiasi kidogo cha mvua pamoja kutokea kwa baridi na joto kali. Miaka milioni iliyopita Karoo ilikuwa na mfumo wa ikolojia wa pekee inayoonekana hado leo katika visukuku vingi.
Hadi leo ni mazingira ya joto kali pamoja na jalidi. Mvua inanyesha kwa wastani milimita 50 hadi 250 kwa mwaka, lakini kwene milima kadhaa hufikia milimita 250 hadi 500. Maji hupatikana chini ya ardhi yanayopatikana kwa njia ya visima vilivyochimbwa.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Karroo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.