Gegereka Kamba

Nusuoda 2 na oda za chini 10:

Kamba
Kamba mwilo (Panulirus longipes)
Kamba mwilo (Panulirus longipes)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Crustacea (Arthropoda wenye miguu yenye matawi mawili)
Ngeli: Malacostraca (Crustacea wenye sehemu tatu)
Oda: Decapoda (Crustacea wenye miguu mikumi)
Ngazi za chini

  • Dendrobranchiata
  • Pleocyemata
    • Achelata
    • Anomura
    • Astacidea
    • Axiidea
    • Brachyura (Siyo kamba lakini kaa)
    • Caridea
    • Gebiidea
    • Glypheidea
    • Polychelida
    • Stenopodidea

Kamba ni wanyama wa faila Arthropoda na oda Decapoda (kutoka Kiyanuni Δεκάποδα: δέκα = kumi, πούς, ποδός = mguu), lakini spishi za oda ya chini Brachyura huitwa kaa. Spishi ndogo huwa na majina kama uduvi, duvi, kijino na ushimbu.

Mwili wa kamba una sehemu mbili: kefalotoraksi (kichwa na kidari vilivyoungana) na fumbatio. Kwa hivyo kamba wana miguu kumi, jozi tano za viungo vya kefalotoraksi, vinavyoitwa pereiopodi pia. Lakini kila pingili ya mwili inaweza kuwa na jozi ya viungo, ijapokuwa vingine vimepotea katika spishi nyingi. Vile vya kichwa ni vipapasio vidogo na vikubwa, mandibuli na maxilla za kwanza na za pili. Jozi ya kwanza ya miguu inabeba magando, pengine madogo pengine makubwa. Kidari kinabeba jozi tatu za viungo mbele ya miguu ambavyo vinaitwa maxillipedi. Viungo hivi vinasaidia kwa kula.

Fumbatio inabeba idadi mbalimbali za viungo vinavyoitwa pleopodi na ambovyo vinatumika kwa kuogelea na kuatamia mayai. Kwa spishi nyingine jozi ya kwanza, na pengine jozi ya pili pia, ya madume imetoholeka ili kumwekea jike manii. Viungo vya pingili ya mwisho huitwa uropodi na mwishoni kwa fumbatio kuna telsoni. Uropodi na telsoni pamoja zinaumba kipepeo cha mkia kinachotumika kwa kutimuka kikikunjwa kwa kasi.

Spishi za Afrika Mashariki zilizochaguliwa

  • Acetes erythraeus, Uduvi-krili madoa-mekundu
  • Aristaeomorpha foliaceae, Kamba mwekundu mkubwa
  • Aristaeopsis edwardsiana, Kamba mwekundu
  • Exhippolysmata ensirostris, Kamba mwindaji
  • Fenneropenaeus indicus, Kamba mweupe Hindi
  • Heterocarpus laevigatus, Uduvi mwekundu
  • Heterocarpus woodmasoni, Uduvi mwekundu Hindi
  • Linuparus somniosus, Kambamawe mkuki
  • Macrobrachium rude, Kamba wa maji baridi
  • Marsupenaeus japonicus, Kamba wa Japani
  • Melicertus canaliculatus, Kamba mchawi
  • Melicertus latisulcatus, Kamba mfalme magharibi
  • Melicertus marginatus, Kamba mfalme wa Hawai
  • Merguia oligodon, Uduvi-mikoko
  • Metanephros andamanicus, Kambamawe wa Andamani
  • Metanephron mozambicus, Kambamawe wa Msumbiji
  • Metapenaeus monoceros, Uduvi madoadoa
  • Metapenaeus stebbeni, Uduvi mhamaji
  • Nephropsis stewarti, Kambamawe wa Stewart
  • Nematopalaemon tenuipes, Kamba-buibui
  • Nephropsis stewarti, Kamba mdogo mwekundu
  • Panulirus homarus, Kamba springi
  • Panulirus longipes, Kamba mwilo
  • Panulirus ornatus, Kamba mwani
  • Panulirus penicillatus, Kamba kijiwe
  • Panulirus versicolor, Kambakulabu
  • Parapenaeopsis acclivirostris, Uduvi pua-kulabu
  • Parapenaeus fissurus, Uduvi pinki
  • Parapenaeus investigatoris, Uduvi pinki
  • Parapenaeus longipes, Uduvi pinki miguu-mirefu
  • Penaeopsis balssi, Uduvi pinki
  • Penaeus monodon, Kambamti mkubwa
  • Penaeus semisulcatus, Kambamti kijani
  • Puerulus angulatus, Kambamawe milia
  • Scyllarides squammosus, Kamba-mzuka butu
  • Scyllarides tridacnophaga, Kamba-mzuka mlashaza
  • Scyllarus batei, Kamba-mzuka laini
  • Scyllarus rugosus, Kamba-mzuka kibyongo
  • Solenocera choprai, Uduvi mgongo-utiko
  • Thenus orientalis, Kamba-mzuka kichwa-bapa
  • Trachysalambria curvirostris, Uduvi manyoya

Picha

Tags:

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

WangoniMbezi (Ubungo)AbrahamuMkoa wa RuvumaMartha MwaipajaHuduma ya kwanzaMkoa wa MorogoroRaiaCristiano RonaldoHistoria ya UislamuAfrikaTanganyika African National UnionNguzo tano za UislamuRohoUundaji wa manenoNgonjeraNgano (hadithi)Wilaya ya KinondoniAgano la KaleNgamiaRupiaMisemoMaambukizi ya njia za mkojoMauaji ya kimbari ya RwandaRushwaUkristoOrodha ya Marais wa ZanzibarUchumiBahari ya HindiJokate MwegeloBibliaSwalaMwanzo (Biblia)PasakaPombeKunguruCleopa David MsuyaBiblia ya KikristoShikamooSimuUyahudiBendera ya TanzaniaKigoma-UjijiMethaliAdolf HitlerUgonjwa sugu wa njia za pumzi zilizofunganaKishazi huruJose ChameleoneOrodha ya viongoziNguruwe-kayaVivumishi vya urejeshiMoses KulolaMkoa wa TaboraMnara wa BabeliMimba kuharibikaInjili ya MarkoShangaziTanzaniaChumba cha Mtoano (2010)Nabii EliyaTanganyikaKukiBiashara ya watumwaSakramentiAlama ya barabaraniMkoa wa SingidaWayahudiShinikizo la juu la damuOrodha ya makabila ya KenyaUkoloniWagogo🡆 More