Windhoek ni mji mkuu wa Namibia, na uko mahali pa 22.56 S 17.09 E.
Idadi ya wakazi wake ni takriban 230,000. Mji huu ni kituo muhimu kwa biashara ya ngozi za kondoo. Zamani ulikuwa makao makuu ya mtemi wa kabila la Nama aliyewashinda kabila la Waherero wakati wa karne ya 19. Mwaka wa 1885, nchi ilivamiwa na wakoloni kutoka Ujerumani, na mji wa Windhoek ukawa makao makuu ya serikali ya ukoloni mwaka wa 1892. Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia nchi ilivamiwa na majeshi ya Makaburu kutoka Afrika ya Kusini ambao wametawala nchi ya Namibia hadi mwaka wa 1990. Namibia ilipopata uhuru, mji wa Windhoek ukawa mji mkuu wa Jamhuri ya Namibia.
Jiji la Windhoek | |
Mahali pa mji wa Windhoek katika Namibia | |
Majiranukta: 22°34′12″S 17°5′1″E / 22.57000°S 17.08361°E | |
Nchi | Namibia |
---|---|
Mikoa | Mkoa wa Khomas |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 400.000 |
Tovuti: www.windhoekcc.org.na |
Makala hii kuhusu maeneo ya Namibia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Windhoek kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Windhoek, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.