Erling Braut Haaland (alizaliwa 21 Julai 2000) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Norway ambaye anacheza kama mshambuliaji wa klabu ya Uingereza Manchester City kwenye Mashindano ya Ligi kuu ya Uingereza na timu ya taifa ya Norway.
Anachukuliwa kuwa ni mmoja wa wachezaji bora zaidi ulimwenguni, anajulikana kwa uchezaji wake, kasi na umaliziaji.
Haaland alizaliwa mnamo 21 Julai 2000 huko Leeds, Uingereza, kwani baba yake Alfie Haaland alikuwa akiichezea klabu ya Leeds United kwenye Ligi ya Klabu bingwa barani Ulaya wakati huo. Mnamo 2004, akiwa na umri wa miaka mitatu, alihamia Bryne, mji ambapo wazazi wake wanaishi huko Norwei.
Pamoja na kucheza kandanda tangu utotoni, Haaland alishiriki katika michezo mingine mbali mbali pindi alikua mtoto, ikiwa ni pamoja na mpira wa mikono,gofu na riadha. Pia inasemekana alipata rekodi ya dunia katika kitengo cha umri wake kwa kuruka kwa umbali mrefu alipokuwa na umri wa miaka mitano, na umbali uliorekodiwa ni mita 1.63 mnamo mwaka 2006.
Håland alianza kazi yake katika klabu ya nyumbani kwake Bryne FK mnamo 2016, na alihamia Molde FK mwaka uliofuata ambapo alitumia miaka miwili. Mnamo Januari 2019 alihamia upande wa Austria Red Bull Salzburg kwa mkataba wa miaka mitano. Alicheza katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya (UEFA) ya 2019-20, alikuwa kijana mdogo kuliko wote kucheza mechi tano mfululizo za Ligi ya Mabingwa ya UEFA.
Mnamo 29 Desemba 2019, Håland alihamia Borussia Dortmund ya Ujerumani kwa ada iliyoripotiwa kuwa € milioni 20.
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Erling Braut Håland kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Erling Braut Håland, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.