Xi'an ni makao makuu ya Mkoa wa Shaanxi nchini China.
Kwenye mwaka 2011 ilikuwa na wakazi milioni 6.
Nchi | China |
Jimbo / Mkoa | Shaanxi |
Anwani ya kijiografia | 34°15′54″N 108°57′14″E |
Kimo | m 405 |
Eneo | km2 1,088 |
Wakazi | 7,135,000 |
Msongamano wa watu | 6,600/km2 |
Simu | 29 |
Tovuti rasmi | www.xa.gov.cn |
Jiji hilo ni maarufu kwa Jeshi la Matofali lililopatikana ndani ya kaburi la kaisari wa kwanza wa China Qin Shi Huang.
Mji huu ulikuwa mji mkuu wa nasaba za wafalme 13, pamoja na nasaba ya Zhou, nasaba ya Qin, nasaba ya Han, nasaba ya Sui, na nasaba ya Tang.
Umuhimu wa mji ulitokana na mahali pake kwenye chanzo cha Barabara ya Hariri iliyounganisha China na Asia ya Magharibi na ya Kusini .
Xi'an inachukuliwa kuwa moja ya taji za kongwe zaidi katika historia ya ulimwengu pamoja na nyingine tatu za Athene, Roma na Cairo.
Xi'an ilijulikana zaidi kwa tahajia ya Sian. Jina la Xi'an lilichaguliwa kwa maana ya "Amani ya Magharibi" wakati wa nasaba ya Ming kwa sababu ilikuwa mji mkubwa kwenye magharibi ya milki ya Ming.
Kama mji wa kihistoria, Xi'an bado imezungukwa na ukuta wa kale. Kivutio kikuu cha wageni ni makaburi ya kifalme pamoja na "jeshi la matofali". Halafu:
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Xi'an, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.