Uchaguzi wa bunge nchini Kenya ulifanyika kama sehemu ya uchaguzi mkuu wa Kenya tarehe 27 Desemba 2007; uchaguzi wa rais ulifanyika tarehe hiyo pia.
| |||||||||||||||||||||||||||||||||||
| |||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Jamhuri ya Kenya |
Makala hii imepangwa kwa mfululizo: |
|
|
Nchi zingine · Atlasi |
Uchaguzi huu wa ubunge ulifanyika ukiwa huru na wa haki kwa ujumla kinyume na uchaguzi wa rais uligombewa vikali. uchalikuwa huu unazingatiwa kuwa wa ajabu kulungana na idadi ya mabadiliko yaliyoshuhudiwa. Miongoni mwa haya yalikuwa:
Bunge la 9 la Kenya lilivunjwa mnamo Jumatatu 22 Oktoba, 2007 Tarehe rasmi ya uchaguzi, ilivyotangazwa na rasmi mnamo 26 Oktoba 2007 na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (ECK), ingekuwa Alhamisi tarehe 27 Desemba 2007. Hii ilimwezesha Spika wa bunge kutoa idhinisho kwa wabunge kuondoka ofisini, hivyo kutangaza nafasi 210 za wabuge wazi. Kisha ECK ilitangaza tarehe ambayo uchaguzi mkuu ungefanyika. Ilivyo kawaida, Wagombezi wanatakiwa kuteuliwa katika chochote kati ya vyama 144 vilivyosajiliwa ili wahitimu kuwa katika uchaguzi. Idadi ya wengi inahitajika kushinda uchaguzi wa bunge. Washindi watakuwa wabunge wateule hadi sherehe rasmi ya kuapishwa kwa Bunge la kumi.
Tume ya Uchaguzi ya Kenya (ECK) ilikuwa awali ya kuweka tarehe ya mwisho 19 Novemba 2007 kwa kuwasilisha orodha ya wanaogombea ili kuzuia khasiri kutoka defecting baada ya kupoteza katika vyama vyao. ECK baadaye iliamua kuruhusu kwa vyama defect kwa madogo ODM, PNU na ODM-K vilifanya uteuzi wao tarehe 16 Novemba, 2007. Orodha ya mwisho ya walikuwa rasmi fram ECK tarehe 23 Novemba, 2007 na 24 Novemba, 2007.
Waziri wa mambo ya ndani wa zamani Chris Murungaru na mshindi wa Tuzo ya Nobel Wangari Maathai walishindwa kushinuteuzi wa chama tawala nchini Kenya ubunge primaries. Maathai alipoteza kat Party of National Unity kuteuliwa na kuamua defect na chama kidogo. Murungaru, mshirika wa karibu wa Kibaki, alipoteza kwa mfanyabiashara asiyejulikana sana.
Mchujo wa pande kuu tatu (ODM, ODM-K na PNU) ul kama chaotic na uligubikwa na makosa na vurugu. wagombea wengi walioshindwa katikka vyama vyao waliihamia vyama vidogo baada ya kushindwa kupata hadhi za ugombezi kwa pande zao
Idadi inayoshikilia rekodi ya wagombea 2548 wangegombea kiti cha ubunge, ikilinganishwa na wagombea 1033 katika uchaguzi uliopita wa bunge mnamo mwaka 2002. Idadi hii imebakia ileile, licha ya idadi ya majimbo (210) Kulikuwa na idadi ya rekodi ya wagombea wanawake, 269.
Chama cha ODM kilikuwa na idadi kubwa zaidi ya wagombea (190), kikifuatiwa na KENDA (170), PNU (135), ODM-Kenya (135), KADDU (97) KANU (91), Safina (88), NARC (73), DP (86) na NARC-Kenya (59). Jumla ya vyama 108 vilikuwa vimewasilisha wagombea ubunge, idadi nyingine ya rekodi Kwa mara ya kwanza katika uchaguzi mkuu wa Kenya, hakuna chama kilichokuwa na mgombea katika kila jimbo. Hapo awali, chama cha KANU kilikuwa kikiwakilishwa na wagombea katika majimbo yote kila wakati.
Eneo Bunge la Kitutu Masaba lilikuwa na idadi kubwa zaidi ya wagombea (33), wote wakigombea kiti kimoja cha ubunge na kila mmoja akiwakilisha chama tofauti mfuatilio. Maeneo bunge yote 210 yangepata angalau wagombea wawili katika kila eneo. Hivyo, kinyume na ilivyokuwa katika uchaguzi mkuu uliopita, hakuna majimbo ambayo yangekuwa na mgombea mmoja
Wagombea wote tisa wa urais pia wangegombea kiti cha ubunge kama inavyotakiwa na sheria ya Kenya. Mshindi wa uchaguzi wa urais lazima pia ashinde kiti cha ubunge ili kutangazwa rais.
Wapiga kura 14,296,180 walikuwa wamejiandikisha kupiga kura. Asilimia 68.8 ya wapiga kura ni umri kati ya miaka 18-40, huku asilimia 31.2 iliyobaki ikiwa watu wakubwa.
Matokeo ya awali yalionyesha kuwa Makamu wa Rais Moody Awori na mshindi wa Tuzo la Amani la Nobel Wangari Maathai walipoteza viti vyao vya ubunge. Wanasiasa wengine mashuhuri waliokuwa na hatima iyohiyo ni Mutahi Kagwe, Musikari Kombo, Simeon Nyachae, Nicholas Biwott, Chris Murungaru, Mukhisa Kituyi, Raphael Tuju, Kipruto Kirwa, Njenga Karume na Gideon Moi, mwana wa rais wa zamani Daniel arap Moi.
Matokeo ya uchaguzi katika maeneo bunge ya Kamukunji, Kilgoris na Wajir Kaskazini yalivutiliwa mbali na uchaguzi katika maeneo hayo ungerudiwa siku zijazo.
Kwa jumla wabunge 207 kati ya 210 walichaguliwa. Kura zikarudiwa katika majimbo 3. Wabunge 12 wa ziada watateuliwa na rais. Akifuata kawaida atawateua kufuatana na nguvu ya vyama bungeni.
Uchaguzi huu ulikuwa na mabadiliko ya ajabu:
Magazeti yalitoa taarifa ya kwamba wabunge 30 wa vyama vidogo waliunda "Kundi la vyama vidogo bungeni" (Small Parties Parliamentary Group); idadi hii ingejumlihsa wabunge waliohesabiwa juu kama kundi la PNU.
ODM | NARC ilishirikishwa na ODM | PNU | Vyama shirikishwa vya PNU | KANU Chama chirikishwa na PNU | ODM-Kenya | Wabunge wanaojitegemea | JUMLA | |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Wabunge | 99 | 3 | 43 | 21 | 14 | 16 | 11 | 207(of 210) |
Vyama shirikishwa vya PNU- KANU (14), Sisi Kwa Sisi (2), Safina (5), NARC-Kenya (4), FORD-Kenya (1), Ford-P (3), New Ford-K (2), Mazingira Party (1), Ford-A (1), DP (2) Wabunge wa kujitegemea waliingia kupitia vyama vidogo kama PDP (1), PPK (1), NLP (1), KADDU (1), UDM (1), PICK (1), CCU (1), Kenda (1) Nation 31-12-2007[dead link] Nation 09-01-2008 Archived 16 Januari 2008 at the Wayback Machine. |
ODM: 5, PNU: 2
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Dagoretti | PNU | Mugo Beth Wambui |
Embakasi | ODM | Were Melitus |
Kasarani | ODM | Elizabeth Ongoro |
Langata | ODM | Odinga Raila Amolo |
Makadara | PNU | Waithaka Dickson Mwangi |
Starehe | ODM | Kariuki Margret Wanjiru |
Westlands | ODM | Gumo Frederick Omulo |
PNU: 18, Safina: 3, KANU: 2, Sisi kwa sisi: 2, FORD-A: 1, FORD-P: 1, PICK: 1 PPK
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Gatanga | PNU | Peter Kenneth |
Gatundu North | PICK | Waibara Clement Kungu |
Gatundu South | KANU | Kenyatta Uhuru |
Gichugu | PNU | Karua Martha Wangari |
Githunguri | SAFINA | Githunguri Baiya Peter Njoroge |
Juja | PNU | Thuo George |
Kandara | PNU | Kamau James Maina |
Kangema | PNU | Michuki John Njoroge |
Kiambaa | KANU | Githunguri Stanley Munga |
Kieni | PNU | Warugongo Namesyus |
Kigumo | PNU | Kamau Jamleck Irungu |
Kiharu | SISI KWA SISI | Mwangi Barnabas Muturi C |
Kikuyu | PNU | Nganga Lewis Nguyai |
Kinangop | SISI KWA SISI | Ngugi David Mwaniki |
Kipipiri | PNU | Kimunya Amos Muhinga |
Kirinyaga Central | FORD A | Kariuki John Ngata |
Lari | PPK | Mwaura David Njuguna Kiburi |
Limuru | FORD P | Mwathi Peter Mungai |
Maragwa | PNU | Elias Peter Mbau |
Mathioya | PNU | Wambugu Clement Muchiri |
Mathira | SAFINA | Maina Ephraim Mwangi |
Mukurweini | SAFINA | Kabando wa Kabando |
Mwea | PNU | Gitau Peter Njuguna |
Ndaragwa | PNU | Kioni Jeremiah Ngayu |
Ndia | PNU | Githae Robinson Njeru |
Nyeri Town | PNU | Mathenge Esther Murugi |
Ol kalou | PNU | Mureithi Erastus Kihara |
Othaya | PNU | Mwai Kibaki |
Tetu | PNU | Nyamo Francis Thombe |
ODM-K: 14, PNU: 7, KANU: 4, CCU: 2, NARC: 2, ODM: 2, DP: 1, NARC KENYA: 1, PICK: 1, SAFINA: 1, Mazingira: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Central Imenti | CCU | Imanyaara Gitobu |
Gachoka | PNU | Mutava Musyimi |
Igembe North | PNU | Ntoitha M'mithiaru |
Igembe South | KANU | Franklin M Linturi |
Isiolo North | NARC KENYA | Mohammed A Kuti |
Isiolo South | KANU | Abdul B Ali |
Kaiti | ODM K | Gideon Ndambuki |
Kangundo | ODM K | Muthama Johnson Nduya |
Kathiani | CCU | Ndeti Wavinya |
Kibwezi | ODM K | Prof Philip Kaloki |
Kilome | PICK | Mwau John Harun |
Kitui Central | NARC | Charity K Ngilu |
Kitui South | ODM K | Muoki Issac Mulatya |
Kitui West | NARC | Nyamai Charles Mutisya |
Laisamis | KANU | Joseph Lekuton |
Machakos Town | ODM K | Victor Munyaka |
Makueni | ODM K | Peter Kiilu |
Manyatta | DP | Emillio Kathuli |
Masinga | ODM K | Itwiku Benson Mbai |
Mbooni | ODM K | Mutula Kilonzo |
Moyale | ODM | Ali Mohamud Mohamed |
Mutito | ODM K | Julius Kiema Kilonzo |
Mwala | ODM K | Pastor Daniel Muoki |
Mwingi North | ODM K | Stephen Kalonzo Musyoka |
Mwingi South | ODM K | David Musila |
Nithi | KANU | Mbiuki Japhet M Kareke |
North Horr | ODM | Francis Chachu |
North Imenti | Mazingira | Ruteere Silas Muriuki |
Runyenjes | PNU | Cecily Mutitu Mbarire |
Saku | ODM K | Sasura Hussein Tarry |
Siakago | SAFINA | Kivuti Maxwell |
South Imenti | PNU | Kiraitu Muriungi |
Tharaka | PNU | Mwiru Alex Muthengi |
Tigania East | PNU | Peter G Munya |
Tigania West | PNU | Kilemi Mwiria Valerian |
Yatta | ODM K | Kilonzo Mutavi Charles |
ODM: 18, PNU: 2, New Ford-K: 2, FORD K: 1, KADDU: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Amagoro | ODM | Ojaamongson Sospeter Odeke |
Budalangi | ODM | Ababu Pius Tawfiq Namwamba |
Bumula | PNU | Bifwoli Sylvester Wakoli |
Butere | ODM | Wycliffe Oparanya |
Butula | ODM | Odhiambo Bwire Alfred |
Emuhaya | ODM | Kenneth Marende |
Funyula | ODM | Nyogesa Otuoma Paul |
Hamisi | ODM | George Haniri |
Ikolomani | NEW FORD KENYA | Dr Bonny Khalwale |
Kanduyi | ODM | Alfred Khang'ati |
Khwisero | ODM | Evans Akula |
Kimilili | FORD K | Simiyu David Eseli |
Lugari | KADDU | Cyrus Jirongo |
Lurambi | ODM | Atanas M Keya |
Malava | NEW FORD KENYA | Soita Peter Shitanda |
Matungu | ODM | David Were |
Mt Elgon | ODM | Fred Kapondi |
Mumias | ODM | Washiali Benjamin Jomo |
Nambale | ODM | Okemo Chrysanthus |
Sabatia | ODM | Musalia Mudavadi |
Shinyalu | ODM | Charles L Lirechi |
Sirisia | PNU | Wentagula Moses Masika |
Vihiga | ODM | Yusuf Kifuma Chanzu |
Webuye | ODM | Sambu B A Wekesa |
ODM: 25, KANU: 2, NARC: 1, NLP: 1, DP: 1, FORD_P: 1, PDP: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Alego | ODM | Yinda Edwin Ochieng |
Bobasi | ODM | Obure Christopher Mogere |
Bomachoge | FORD P | Joel Onyancha |
Bonchari | ODM | Onyancha Charles |
Bondo | ODM | Oginga Dr Oburu |
Gem | ODM | Midiwo Washington Jakoyo |
Gwassi | ODM | Ng'ongo Mbadi John |
Karachuonyo | ODM | Rege James G Kwanya |
Kasipul Kabondo | ODM | Magwanga Joseph Oyugi |
Kisumu Rural | ODM | Nyong'o Peter Anyang' |
Kisumu Town East | ODM | Ahmed Shakeel shabbir Ahmed |
Kisumu Town West | ODM | Aluoch John Olago |
Kitutu Chache | PDP | Richard Momoima |
Kitutu Masaba | NLP | Osebe Walter Enock Nyambati |
Kuria | DP | Machage Wilfred Gisuka |
Mbita | ODM | Kajwang Gerald Otieno |
Migori | ODM | Dache John Pesa |
Muhoroni | ODM | Olweny patrick Ayiecho |
Ndhiwa | ODM | Ojodeh Joshua Orwa |
North Mugirango Burabu | KANU | Ombui Moriasi Wilfred |
Nyakach | ODM | Anyango Pollyins Ochieng |
Nyando | ODM | Otieno Frederick Outa |
Nyaribari Chache | NARC | Monda Robert Onsare |
Nyaribari Masaba | KANU | Ongeri Samson Kagengo |
Nyatike | ODM | Anyanga peter Edick Omondi |
Rangwe | ODM | Ogindo Martin Otieno |
Rarieda | ODM | Gumbo Nicholas O |
Rongo | ODM | Otieno Dalmas Anyango |
South Mugirango | ODM | Magara James Omingo |
Ugenya | ODM | Orengo Aggrey James |
Uriri | ODM | Cyprian Ojwang Omollo |
West Mugirango | ODM | Gesami James Ondicho |
ODM: 12, PNU: 3, NARC-K: 2, ODM-K: 1, FORD-P: 1, KADU ASILI: 1, KANU: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Bahari | ODM | Gunda Benedict Fodo |
Bura | ODM K | Abdi Nassir Nuh |
Changamwe | ODM | Kajembe Ramadhan Seif |
Galole | ODM | Godhana Dhadho Gaddae |
Ganze | KADU ASILI | Bayah Francis S.K |
Garsen | NARC KENYA | Danson Mungatana |
Kaloleni | PNU | Kambi Samwel Kazungu |
Kinango | FORD P | Rai Samuel Gonzi |
Kisauni | ODM | Joho Hassan Ali |
Lamu East | PNU | Abuchiaba Abu Mohamed |
Lamu West | NARC KENYA | Twaha Fahim Yasin |
Likoni | ODM | Mwahima Mwalimu Masudi |
Magarini | ODM | Jeffah Amason Kingi |
Malindi | ODM | Mung'aro Maitha Gideon |
Matuga | PNU | Mwakwere Chirau Ali |
Msambweni | ODM | Zonga Omar Mbwana |
Mvita | ODM | Balala Najib Mohamed |
Mwatate | ODM | Mwatela Calist Andrew |
Taveta | KANU | Shaban Naomi Namisi |
Voi | ODM | Mwakulegwa Danson Mwazo |
Wundanyi | ODM | Mwadeghu Thomas Ludindi |
ODM: 32, PNU: 11, Kanu: 1, Kenda: 1, NARC-K: 1, UDM: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Ainamoi | ODM | David Too Kimutai |
Aldai | ODM | Dr Sally Kosgey |
Baringo Central | ODM | Mwaita Sammy Silas Komen |
Baringo East | PNU | Kamama Asman Abongutum |
Baringo North | ODM | William Kipkorir |
Belgut | ODM | Charles K. Cheruiyot |
Bomet | ODM | Kipkalya Kones |
Bureti | ODM | Bett Franklin |
Chepalungu | ODM | Isaac Ruto |
Cherangani | ODM | Joshua Kutuny |
Eldama Ravine | ODM | Lessonet Moses K |
Eldoret East | ODM | Kamar Margret Jepkoech |
Eldoret North | ODM | Ruto William Samoei |
Eldoret South | ODM | Peris Chepchumba |
Emgwen | ODM | Lagat Elijah Kiptarbei |
Kacheliba | ODM K | Samuel Poghisio |
Kajiado Central | ODM | Joseph Ole Nkaissery |
Kajiado North | PNU | Saitoti George |
Kapenguria | ODM | Rev Julius Mugor |
Keiyo North | ODM | Chepkitony Lucas Kipkosei |
Keiyo South | ODM | Kiptanui Kiplagat Jackson |
Kipkelion | ODM | M J Kiprono Langat |
Konoin | ODM | Kones Julius Kipyegon |
Kuresoi | ODM | Zakayo Cheroiyot |
Kwanza | PNU | Dr Noah Wakesa |
Laikipia East | PNU | Kiunjuri Festus Mwangi |
Laikipia West | PNU | Muriithi Ndiritu |
Loitoktok | NARC KENYA | Katoo Ole Metito |
Marakwet East | KENDA | Kilimo Jebii Linah |
Marakwet West | ODM | Kaino Boaz Kipchuma |
Mogotio | UDM | Prof Hellen Sambili |
Molo | PNU | Kiuna Joseph Nganga |
Mosop | ODM | Koech David |
Naivasha | KANU | Mututho John Michael Njenga |
Nakuru Town | PNU | Lee Maiyani Kinyanjui |
Narok North | ODM | Ntimama William Ronkorua |
Narok South | ODM | Nkoidilla Lankas |
Rongai | ODM | Kigen LukaKipkorir |
Saboti | PNU | Eugene Ludovic Wamalwa |
Samburu East | ODM | Lentimalo Raphael |
Samburu West | ODM | Simon Lesirma |
Sigor | ODM | Wilson Litole |
Sotik | ODM | Lorna Chepkemoi Laboso |
Subukia | PNU | Nelson R Gaichuhie |
Tinderet | ODM | Kosgey Henry Kiprono |
Turkana Central | PNU | David E Ethuro |
Turkana North | PNU | John Munyes |
Turkana South | ODM | Josephat Koli Nanok |
Kanu: 4, ODM: 5; Safina: 1
Jimbo la uchaguzi | Chama | Aliyechaguliwa |
---|---|---|
Dujis | ODM | Duale Aden Bare |
Fafi | KANU | Sugow Aden Ahamed |
Ijara | KANU | Haji Mohamed Yussuf |
Lagdera | ODM | Farah Maalim |
Mandera Central | SAFINA | Abdikadir Hussein Mohamed |
Mandera East | ODM | Mohamed Hussein Ali |
Mandera West | ODM | Maalim Mahmud Mohamed |
Wajir East | ODM | Mohamed Ibrahim Elmi |
Wajir South | KANU | Abdirahman Ali Hassan |
Wajir West | KANU | Wehiye Adan Keynan |
Kufuatia uchaguzi, wabunge wawili wa ODM- Mugabe Were na David Kimutai Too -waliuawa wakati wa mgogoro baada ya uchaguzi, ambao ulitokana na mzozo juu ya matokeo ya uchaguzi wa rais. Kufuatia vifo hivi, uchaguzi mmdogo ulihitajika katika majimbo yao; zaidi ya hayo, uchaguzi ulikuwa ufanyike katika majimbo mawili Mkoani Rift Valley ambako matokeo hayakutangazwa kamwe kutokana na vurugu. Kenneth Marende alichaguliwa kuwa Spika wa Bunge kufuatia uchaguzi, hivyo kuacha kiti chake wazi na kuhitaji uchaguzi mwingine ufanyike katika jimbo lake. Kufikia wakati huu, chama cha ODM kiliachwa na viti 96.
Uchaguzi mdogo katika maeneo haya matano ulifanyika mnamo tarehe 11 Juni 2008. Mnamo 10 Juni, mawaziri wawili-Waziri wa Barabara Kipkalya Kones na Naibu Waziri wa Maswala ya Nyumbani Lorna Laboso, wote kutoka ODM-waliuawa katika mlipuko wa ndege, na kuacha viti vingine viwili wazi (na kupunguza viti vya ODM hadi wabunge94). [onesha uthibitisho] Wabunge hao walikuwa wakienda mkoa wa Bonde la Ufa kwa ajili ya uchaguzi mdogo wakati ajali hiyo ilitokea.
ODM ilishinda uchaguzi mdogo katika majimbo matatu kati ya matano, huku PNU ikishinda katika maeneo mawili. ODM ilihifadhi viti vyake katika maeneo bunge ya Emuhaya na Ainamoi, lakini, ikupoteza kiti cha Embakasi jijini Nairobi kwa PNU. Kufikia sasa ODM ina wabunge 103 huku PNU ikiwa na wabunge 104 wanaoziegemea pande hizi mbili mtawalia.
Uchaguzi mdogo ulifanyika katika majimbo ya Bomet na Sotikmnamo 25 Septemba na ulishindwa na Beatrice Kones na Joyce Laboso mtiririko huo. Viti vilihifadhiwa na ODM na washindi walikuwa jamaa wa karibu wa watangulizi wao, ambao walikufa katika ajali ya ndege Juni: Beatrice Kones ni mjane wa Kipkalya Kones na Joyce Laboso ni dadake Lorna Laboso
Mnamo Mei 2009, Bunge lilihidhinisha kuundwa kwa Tume huru ya Uchaguzi ya mpito (IIEC), iliyosimamia uchaguzi mdogo katika majimbo ya Shinyalu na Bomachoge, ambao ulifanyika tarehe 27 Agosti 2009. Kiti cha Shinyalu kilibaki wazi wakati aliyekuwa mbunge wake Charles Lugano wa ODM aliaga dunia. ODM ilihifadhiwe kiti hicho, kufuatia ushindi wa Justus Kizito katika uchaguzi huo mdogo. Kiti cha Bomachoge pia kiliachwa wazi mara baada ya Uchaguzi wa 2007 katika jimbo kuvutiliwa mbali kufuatia udanganyifu. Kiti hiki kilikuwa kimeshindwa Joel Onyancha wa chama cha Ford-People katika uchaguzi mkuu wa 2007. Katika uchaguzi huu mdogo wa 2007 Simon Ogari wa ODM aliipuka mshindi huku akifuatwa kwa karibu na Joel Onyancha, ambaye wakati huu alikuwa akiwakilisha PNU Kwa mara ya kwanza nchini Kenya, vijisanduku vya uchaguzi vilivyotumikavilikuwa vimeundwa kwa kutumia vifaa vya uwazi (mtu angeweza kuona ndani ya vijisanduku)
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uchaguzi wa bunge nchini Kenya, 2007, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.