Ngeli 2 na nusungeli 2
Mnyoo-bapa | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mnyoo-bapa wa maji baridi (Planaria torva) | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
|
Minyoo-bapa ni wanyama wanaofanana na minyoo, lakini wao hawana uwazi wa mwili (coelom). Kwa hivyo hawana ogani za mfumo wa mzunguko wa damu au za mfumo wa upumuaji na lazima mwili uwe bapa ili oksijeni iweze kuingia kwa mtawanyiko. Mwili wao una uwazi umoja, ule wa mmeng'enyo, lakini uwazi huu una kipenyo kimoja tu pamoja kwa umezaji na kwa utoaji.
Kuna minyoo-bapa ambao huishi kwa maji au kwa udongo. Kwa kawaida hawa hula wanyama wadogo lakini pia wanyama wakubwa kuliko wao wenyewe, kama konokono. Zaidi ya nusu ya spishi zote za minyoo-bapa ni vidusia, k.m. mategu. Hawa hufyonda virutubishi vilivyoyeyuka katika giligili za mwili wa mwenyeji.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mnyoo-bapa, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.