Derg ni neno la Kiethiopia kwa ajili ya kamati au halmashauri.
Inamaanisha hasa kikundi cha wanajeshi waliompindua Kaisari Haile Selassie mwaka 1974 na kushika mamlaka ya serikali nchini Ethiopia.
Derg ilikuwa kamati ya wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za jeshi kama jeshi la nchi kavu, wanamaji, wanaanga na polisi. Derg ilitawala hadi 1987.
Kati ya 1975 na 1977 watu makumi elfu waliuawa hovyo kwa amri za Derg.
Mwenyekiti na kiongozi mkuu wa Derg alikuwa Mengistu Haile Mariam.
1987 Derg ilikabidhi madaraka kufuatana na katiba mpya na Ethiopia kutangazwa kuwa jamhuri ya kisoshalisti na Mengistu rais wake.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Derg, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.