Binti ni filamu ya kuigiza ya Tanzania ya mwaka 2021 iliyoongozwa na Seko Shamte na kutayarishwa na mkurugenzi mwenyewe na Alinda Ruhinda na Angela Ruhinda.
Waigizaji nyota wa filamu hii ni Bertha Robert, Magdalena Munisi, Helen Hartmann na Godliver Gordian katika nafasi kuu huku Yann Sow, Alex Temu na Jonas Mugabe wamecheza nafasi za wasaidizi.
Filamu hii inahusu hali ya wanawake wa kisasa jijini Dar es Salaam katika sura nne: Tumaini, Angel, Stella na Rose.
Filamu hiyo imerekodiwa ndani na nje ya jiji la Dar es Salaam, Tanzania. Marekebisho ya rangi yalifanyika India na jiji la Los Angeles, na sauti ilifanyika Misri.
Onyesho la kwanza la filamu hii lilicheleweshwa kwa miaka miwili kwa sababu ya janga la UVIKO-19.
Filamu hii ni ya kwanza ya Kitanzania kuonyeshwa Netflix.
Makala hii kuhusu filamu fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Binti (filamu ya 2021) kama waigizaji wake, hadithi au matoleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Binti (filamu ya 2021), which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.