Neema Mduma (alizaliwa mkoani Morogoro, 21 Oktoba 1989 (1989-10-21) (umri 34) ni mwanazuoni, daktari aliyebobea kwenye taaluma ya sayansi na teknolojia.
Ni moja kati ya Watanzania waliowahi pata Udaktari wa Filosofia (PhD) katika umri mdogo na kati ya watu wenye kuwatia ari mabinti wengine katika masuala ya elimu, hususani masomo yenye kuhusisha sayansi na hesabu.
Neema Mduma | |
Amezaliwa | 21 Oktoba 1989 Morogoro |
---|---|
Nchi | Tanzania |
Kazi yake | Mhadhiri Mwandamizi |
Mwajiri | Nelson Mandela African Institution of Science and Technology |
Elimu | Shahada ya Uzamivu (PhD) |
Dini | Mkristo |
Dhehebu | Mlutheri |
Ndoa | Ameolewa |
Mwenza | Hudson Laizer |
Wazazi | Baba: Mathias Mduma Mama: Judith Tesha |
Tovuti | https://nm-aist.ac.tz |
Neema, ambaye kikabila ni Mpare na baba yake ni mchungaji wa kanisa anaye fahamika kwa jina la Mathias Mduma na mama yake ni mwalimu anaye fahamika kwa jina la Judith Tesha. Alisoma awali katika shule ya msingi Bungo iliyopo mjini Morogoro kuanzia mwaka 1996 mpaka mwaka 2002. Kuhitimu kwake darasa la saba kukampa nafasi ya kuchaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari Kilakala Sekondari ambayo ni shule ya vipaji maalumu kwa wasichana. Hivyo alianza kidato cha kwanza mwaka 2003 na kuhitimu kidato cha nne mwaka 2006 na kuendelea na kidato cha tano mwaka 2007 na kuhitimu kidato cha sita mwaka 2009 hapo hapo Kilakala.
Mwaka 2009 alipata nafasi ya kujiunga na masomo ya elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Iringa (zamani Tumaini) na kuanza masomo ya shahada ya kwanza na alisomea shahada ya Sayansi ya Habari na Mawasiliano. Mara baada ya kumaliza shahada hiyo alijiunga na taasisi ya NM-AIST na kuendelea na shahada ya sayansi ya uzamili (MSc) na baadae shahada ya uzamivu (PhD) kwenye mambo ya sayansi na teknolojia ya mawasiliano akibobea katika masuala ya Akili Mnembe (Artificial Intelligence).
Neema zaidi ya kuwa na mapenzi na elimu, ni mtafiti mzuri na amekuwa akishirikiana na watafiti wenzake katika kutafuta namna mbali mbali za kuweza tatua changamoto za kijamii. Mfano wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, Neema alishirikiana na wenzake kutoka Kenya na Uganda na kuweza fanikiwa pata fedha ya kuwawezesha kufanya utafiti katika kada za kilimo, elimu na afya.
Mara baada ya kumaliza masomo, Neema aliajiriwa kama Mkufunzi msaidizi katika Chuo Kikuu cha Iringa kuanzia mwaka 2012 hadi mwaka 2017 kisha akajiunga na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela ambapo alifanikiwa kuajiriwa na kuwa Mhadhiri msaidizi na baadae kama Mhadhiri, na tarehe 23 mwezi wa pili mwaka 2024 Neema alipandishwa daraja kutoka Mhadhiri na kuwa Mhadhiri mwandamizi baada ya kukidhi vigezo vya kufundisha, kufanya tafiti na kutoa machapisho ya kisayansi.
Neema akiwa anamalizia masomo yake ya uzamivu (PhD), aliamua kufanya utafiti na kujikita katika kutafuta suluhisho la kudumu ili kuweza tatua tatizo la utoro mashuleni wenye kupelekea wanafunzi kufeli katika masomo yao au kuacha shule kabisa. Hivyo alitengeneza mfumo ulio itwa Baki shule. Mfumo huu unatumia akili mnembe katika kutambua viashiria vya utoro ulio kithiri ama dalili za utoro kwa mwanafunzi au wanafunzi na kuweza wasaidia wazazi na walimu kutambua mapema kabla tatizo halija kithiri na kuathiri ufaulu wa mtoto darasani.
Ili kuweza saidia jamii ya Kitanzania, Neema hutumia muda wake wa ziada kukutana na mabinti mashuleni na kuweza zungumza nao kuhusu masomo ya Sayansi na Hesabu huku akitoa mafunzo ya kuandika mistari ya Codes zenye kufanya Kompyuta kutenda jambo fulani. Elimu hii huwasaidia mabinti kuweza penda masomo ya Sayansi na Hesabu hivyo kuweza timiza ndoto zao za kuwa Wanasayansi kama Neema au kwenda mbali zaidi.
Matumizi ya "Machines Learning" kwenye Elimu, Kilimo na Afya
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Neema Mduma, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.