Jamhuri ya Shirikisho ni muundo wa kisiasa ambako jamhuri hutazamiwa kama maungano wa maeneo ndani yake -kwa kawaida huitwa majimbo- yenye haki zao zisizopewa wala zisizonyanganywa na serikali kuu ya kitaifa.
Katika muundo huu taifa hatawaliwi na serikali moja katika mambo yote lakini madaraka hugawiwa kati ya madaraka ya serikali ya kitaifa na madaraka ya majimbo.
Mara nyingi maazimio kuhusu mambo ya utamaduni hubaki kwenye ngazi ya jimbo lakini pia sehemu za kodi na sisasa ya kiuchumi. Siasa ya nje na mambo ya jeshi hushikwa na serikali kuu. Mambo mengine hutegemea na utaratibu wa kikatiba katika kila nchi.
Mifano ya jamhuri za shirikisho:
Si lazima ya kwamba kila shirikisho ni jamhuri. Mifano ya falme ya shirikisho ni Falme za Kiarabu na Malaysia; kihistoria pia Dola la Ujerumani hadi 1918.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jamhuri ya shirikisho, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.