Balbu (pia: globu; kutoka Kiing.
Hutumiwa kama sehemu ya kifaa kikubwa zaidi kama taa ya umeme.
Balbu hufanya kazi yake kwa kipindi fulani tu baadaye inakwisha inahitaji kubadilishwa. Wakati wa kutoa nuru inashika joto na kwa balbu zenye uzi joto hii huwa na kiwango cha kumwumiza mtu anayeigusa. Ikibadilishwa ni lazima kuangalifu maana inawezekana kupigwa na umeme kama mtu anagusa soketi yaani upande wa taa inayoshika balbu.
Balbu ya kutolea nuru iligunduliwa katika karne ya 19. Awali waya nyembamba ya platini iliwekwa ndani ya gimba la kioo lililoondolewa hewa yote; wakati umeme ulipitishwa kwenye waya hii ilipashwa joto hadi kutoa nuru. Balbu za kwanza hazikudumu muda mrefu kwa hadi Thomas Edison alifauli kuziboresha kwa kutumia nyaya za kaboni au aloi mbalimbali za metali na kujaza balbu kwa gesi kama arigoni au nitrojeni iliyozuia kuharibika haraka kwa nyaya za kung'aa. Tangu wakati wake taa za umeme zilianza kusambaa kote duniani zikabadilisha maisha ya watu kwa kuwapa uwezekano wa kuangaza nyumba na barabara wakati wowote kwa gharama ndogo.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Balbu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.